Panya “Watakatifu”
◆ Hekalu la Deshnouk, lililo katika mkoa wa India wa Rajasthan, limewekwa wakf kwa panya. Inasemekana kwamba katika mahali hapo panya hao “watakatifu” wanalishwa kila mwaka nafaka yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 24. Mhaji akimkanyaga panya “mtakatifu” na kumwua bila kukusudia, anaadhibiwa. Faini anayotolewa ni nini? Ni kutoa zawadi ya sanamu ya dhahabu ya kiumbe huyo aliyekufa yenye gharama ya karibu shilingi 3,600. Akifikiria nafaka wanayolishwa panya hao katika Deshnouk, mwanasayansi wa India Narendra Sharma aliuliza hivi: “Hicho si kinyume cha mambo? Imekuwaje hata panya wenye afya wanatembea-tembea vitumbo vyao vikiwa vimejaa vitu vizuri-vizuri vyote katika mkoa wenye njaa kwa muda mrefu sana ambako wanadamu hata hawawezi kutazamia kuwa na wakaa za chakula zenye kusawazika kwa siku?”