Je! Unakumbuka?
Je! umesoma matoleo ya karibuni ya Mnara wa Mlinzi kwa uangalifu? Ikiwa ndivyo, bila shaka utayakumbuka mambo haya:
● Je! ahadi ya Mungu inayosema ataondoa “maumivu” ina maana ya kwamba maumivu yote yatakwisha?—Ufu. 21:4.
Hapana, kuona maumivu kunasaidia mtu aone hatari, afanye haraka ajiepushe na kitu kinachomwumiza. Inaposemwa kwamba maumivu “hayatakuwapo,” maana ni kwamba mambo yenye kutaabisha mwanadamu, yaani, uonezi, uhalifu, magonjwa, kifo na mengineyo, yataondolewa duniani.—M 9/15/77 415.
● Ni wakati gani kuchagua kukaa bila kuoa au kuolewa kunapoletea mtu faida nyingi?
Kukaa bila kuoa au kuolewa kunaletea mtu faida ikiwa sababu yake ya kukaa hivyo ni ya kiroho, ikiwa anakaa hivyo akitaka kutumia wakati mwingi zaidi atumikie watu na kuwasaidia waipate thawabu kuu ya uzima wa milele.—M 9/15/77 411.