Kuhudhuria Mikutano Kunasaidia Mtu Akomae Upesi
JAMAA moja katika Fagaalu, American Samoa, ilikubali mwaliko wa kujifunza Biblia na wamisionari wa Mashahidi wa Yehova. Ni mara chache sana waliopata kukosa funzo lao la Biblia la nyumbani, walakini, hawakuona uhitaji wa kuhudhuria mikutano ya kundi. Wao waliona kwamba funzo lao la faragha nyumbani mwao lilitosha. Siku moja yule mmisionari alitaka kuwaonyesha kwamba wanahitaji kuhudhuria mikutano. Alileta karatasi ya mtihani wa kuandika ya Shule ya Kitheokrasi, inayofanywa kila juma katika Jumba la Ufalme. Watu hawa wawili hawakujua mengi ya majibu ya maswali hayo. Walielezwa kwamba wakihudhuria mikutano hiyo watafaidika sana katika njia nyingi, mojawapo ikiwa mtihani wa kuandika. Ndipo jamaa hiyo ilipofanya jitihada za kufika katika mikutano. Leo hesabu fulani ya washiriki wa jamaa hii imebatizwa nao wanatia bidii sana katika kazi ya kueneza habari njema za Ufalme kwa wengine.