Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w79 5/15 uku. 24
  • “Kikapu cha Matunda ya Wakati wa Hari”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Kikapu cha Matunda ya Wakati wa Hari”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
w79 5/15 uku. 24

“Kikapu cha Matunda ya Wakati wa Hari”

Nyakati nyingine Yehova Mungu aliwapelekea manabii wake ujumbe kwa njia ya mifano myepesi. Mfano wa hili unapatikana katika Amosi 8:​1-3, tusomapo hivi: “Haya ndiyo aliyonionyesha Bwana [Yehova]; tazama, kikapu cha matunda ya wakati wa hari. Akaniambia, Amosi, unaona nini? Nikasema, Naona kikapu cha matunda ya wakati wa hari. Ndipo [Yehova] akaniambia, Mwisho wao umewajilia watu wangu Israeli; sitawapita tena kamwe. Tena nyimbo za hekaluni zitakuwa vilio siku ile, asema Bwana [Yehova]; mizoga itakuwa mingi; kila mahali waitupa, wakinyamaza kimya.”

Katika maandishi ya Kiebrania usemi “matunda ya wakati wa hari” (“qayits”) na “mwisho” (“qets”) unafanana sana, ukifanyiza mchezo wa maneno. “Kikapu cha matunda ya wakati wa hari” huonyesha uhakika wa kwamba mavuno, na kwa hiyo, mwaka wa kilimo, unakaribia kumalizika. Vivyo hivyo, Israeli wasioaminika walielekea mwisho wao. Yehova Mungu hangeweza tena kusamehe dhambi za watu hao. Afikilizapo hukumu yake, nyimbo za sifa zilizokuwa zikiimbwa hekaluni zingekuwa “vilio,” ombolezo kubwa juu ya wengi waliouawa. Kwa sababu ya wonyesho huu wenye kuogopesha sana wa hasira ya Mungu, jambo peke yake lililofaa ni kunyamaza kimya.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki