Huenda Ulikosa Miaka Yetu ya Kwanza 100 Moja Lakini Usikose Miezi 12 ijayo
Gazeti unaloshika mkononi mwako lilianzishwa livute fikira kwenye mambo yanayotabiriwa na Biblia kwa siku zetu. Na kwa sababu hiyo mara nyingi Mnara wa Mlinzi unakuwa wa kwanza kutaja mambo.
◆ Mapema sana katika mwaka 1879, ulionya ulimwengu juu ya hatari iliyokuwa ikija katika mwaka 1914.
◆ Ulifunua wazi kwamba mengine ya mafundisho ya kidini yaliyoenea pote hayakuungwa mkono na Biblia. Ulizima moto wa hell (Mhu. 9:5); ukathibitisha kwamba nafsi inakufa (Eze. 18:4, NW); ukaonyesha kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu, wala si Mungu Mwenye Nguvu Zote.—Marko 13:32.
◆ Katika mwaka 1920, Ushirika wa Mataifa ulipokuwa bado unaundwa, ulionyesha kile Biblia ilichokuwa imesema kingeupata; na katika mwaka 1942, hatua zilipokuwa zikichukuliwa kuunda Umoja wa Mataifa, ulivuta fikira kwenye matokeo yaliyoonyeshwa na unabii wa Biblia kuuhusu.—Ufu. 17:8-11.
◆ Kwa kutumia Mathayo 24, si kwamba tu uliwatayarisha wasomaji wake juu ya siku zenye hatari na zenye matendo ya uasherati na jeuri yanayozidi kuongezeka katika kizazi hiki, bali pia unatukumbusha juu ya ufumbuzi unatolewa na Mungu—serikali yake ya Kifalme.
◆ Unajitahidi sana kuwa chanzo cha faraja ukikumbusha watu kanuni za Biblia za kuunganisha jarnaa, kushikamana na adili na kushika ukamilifu kibinafsi.
Waweza kuuandikisha katika yo yote ya lugha 82 zinazoonyeshwa katika ukurasa wa pili.
Tafadhali nipelekeeni Mnara wa Mlinzi (matoleo 24 kwa mwaka). Nimetuma shilingi 20.00. (6Z).