Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w80 2/15 kur. 19-22
  • Roho Takatifu Kama Mwombezi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Roho Takatifu Kama Mwombezi
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
w80 2/15 kur. 19-22

Roho Takatifu Kama Mwombezi

1, 2. (a) Wakristo wanahitaji roho takatifu kama mwombezi wakati wanapokuwa chini ya hali gani?

ZAIDI ya kuwa mshuhudiaji kwa watoto wa Mungu wa kiroho, nguvu hii takatifu ya utendaji inatimiza kusudi jingine. Mtume Paulo anavuta fikira juu ya kusudi hili katika barua yake aliyoliandikia kundi katika Rumi, ambalo, kama vile asemavyo Paulo, washiriki wake walikuwa Wakristo “walioitwa kuwa watakatifu,” hawa wakiwa vilevile “warithi kweli wa Mungu, lakini warithi washirika pamoja na Kristo.” (Rum. 1:7; 8:16, 17, NW) Paulo anaandika hivi:

“Wala si hivyo tu; ila na sisi wenyewe tulio na malimbuko ya [r]oho, sisi pia tunaugua katika nafsi zetu, tukikutazamia kufanywa wana, yaani, ukombozi wa mwili wetu. Kwa maana tuliokolewa kwa [tumaini]; lakini kitu ki[lichotumainiwa] kikionekana, hakuna [tumaini] tena. Kwa maana ni nani [anayekitumainia] kile akionacho? Bali [tukitumainia] kitu tusichokiona, twakingojea kwa saburi.”

‘Kadhalika roho nayo hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo; lakini, roho yenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa. Na yeye aichunguzaye mioyo aijua nia ya roho ilivyo, kwa kuwa huwaombea watakatifu kama apendavyo Mungu.’​—Rum. 8:23-27.

2 Kuhusiana na jambo hili maneno ya Mithali 13:12 yanafaa sana: “Kilichotarajiwa kikikawia kuja, moyo huugua.” Wakiwa kati ya kuumba huku kwa kibinadamu kunakougua, Wakristo watoto wa kiroho wa Mungu wanatumainia ukombozi wao kutokana na mwili wa kibinadamu usiokamilika na kuingia kwenye urithi wao wa kimbinguni. Nyakati nyingine inakuwa vigumu kwao kusema waziwazi na Mungu katika sala, kwa kutojua jambo la kuomba wanapokuwa chini ya hali zenye magumu. Ndipo wanapohitaji mwombezi, yaani, roho takatifu ya Mungu.

3, 4. (a) Kwa habari ya waandikaji wa Maandiko ya Kiebrania, sababu gani ilikuwa kama kwamba roho takatifu ndiyo iliyokuwa ikisema na kuandika? (b) Waandikaji hao wa Biblia Waebrania wanalinganaje na washiriki wa kundi la Kikristo kwa habari ya maono ya ndani na udhaifu?

3 Mtume Paulo asema kwamba “sisi wenyewe,” yaani, Paulo na ndugu zake Wakristo waliozaliwa kwa roho ya Mungu, ‘wana malimbuko, yaani, roho.’ (Rum. 8:23) Hapa Paulo anamaanisha kwamba walikuwa na nguvu takatifu ya utendaji ya Mungu isiyoonekana. Nguvu hii ya utendaji imeongoza wanaume waseme na kuandika yale waliyosema. Ilikuwa kama kwamba roho yenyewe ndiyo iliyokuwa ikisema na kuandika. Kupatana na ukweli huu, twasoma hivi: “Hakuna unabii katika maandiko upatao kufasiriwa kama apendavyo mtu fulani tu. Maana unabii haukuletwa po pote kwa mapenzi ya mwanadamu; bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu, wakiongozwa na [roho takatifu].” (2 Pet. 1:20, 21) Maandiko ya Kiebrania yaliyoongozwa kwa roho ambayo kutoka hayo Paulo alitumia maneno yake ili autetee Ukristo yaliandikwa na wanadamu wa vivi hivi tu. Walikuwa na maono yale yale ya moyoni pamoja na udhaifu wa mwili walio nao washiriki wa kundi la Kikristo. Kwa hiyo twaweza kujisikia kama vile walivyojisikia kwa habari hii:

4 “Sisi nasi tu wanadamu hali moja na ninyi.” Akasema mtume Paulo akiwa pamoja na Barnaba mmisionari mwenzake kwa wapagani wenye kuabudu sanamu waliowadhania kuwa watu wenye nguvu zipitazo za binadamu, miungu waliowatokea wanadamu kwa miili ya nyama.​—Matendo 14:15.

5. (a) Kwa kweli maandishi ya Biblia ni semi za nguvu gani, na kwa hiyo yanafaaje? (b) Hali za watu waliotajwa katika Biblia zilihusu sehemu gani zilizohitaji msaada upitao wa kibinadamu?

5 Kwa kweli maandishi hayo ya Biblia yaliyoongozwa kwa roho ya Mungu yalikuwa semi za roho takatifu ya Mungu. Kwa sababu hiyo maandishi hayo yaliyoongozwa na Mungu “[yanafaa] kwa mafundisho, na kwa kuwaadibisha katika haki; ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema.” (2 Tim. 3:16, 17) Zilizotiwa ndani ya maandiko hayo ‘yenye kufaa’ ni sala zilizotolewa Mungu, na ambazo hazikutolewa na waandikaji wa Biblia peke yao, bali vilevile na watu wengine waliojitoa kwa Yehova Mungu. Sala hizi zimetolewa Mungu katika hali za kila namna. Watu hao waliokuwa na udhaifu wa kibinadamu unaotupata sisi sote waliona mikazo ya hali za pekee na zenye hatari zilizokuwapo. Hali zao zenye uhitaji zilikuwa za namna mbalimbali hivi kwamba zatosha kulingana na hali ambazo huenda Wakristo wa kweli wa leo wakakutana nazo nyakati nyingine. Hivi huwa visa ambavyo msaada unaopita wa kibinadamu wahitajiwa. Hivyo, basi, sisi tutasalije?

6, 7. (a) Kwa hiyo Wakristo wanapata hasara gani kwa kutojua namna ya kusali? (b) Hivyo, basi, roho iliyoongoza kuandikwa kwa Biblia inawaombeaje Wakristo, naye Mungu anafahamuje na kujibuje?

6 Katika udhaifu wetu na kutojua la kufanya, “sisi pia tunaugua katika nafsi zetu.” (Rum. 8:23) Hatujui namna ya kumsihi Mungu kwa maneno yaliyotungwa sawasawa au tumwambie nini Msaidizi wetu wa kimbinguni. Hata hivyo, Mungu anaifahamu hali yetu naye anatambua sawasawa yale hasa tunayotamani kwa unyofu kupata.

7 Ikiwa sisi wenyewe hatuwezi kutunga sala, basi, sala zimekwisha tungwa kwa ajili yetu. Wapi? Katika Maandiko Matakatifu ya kiunabii yaliyoongozwa kwa roho ya Mungu. Mungu anafahamiana kabisa na sala zilizoandikwa katika Neno lake. Yeye anajua “nia” (au “maana,” NW) yazo. Yeye anajua zile zinazotufaa sisi tunaotaka kusali ifaavyo. Kwa hiyo Mungu huziona sala hizo zinazofaa zilizoandikwa kana kwamba zinatolewa na Wakristo hao wanaougua wenyewe. Sala hizo hazikutolewa na Wakristo hao wenye uhitaji wenyewe, walakini Mungu huzisikiliza kama kwamba roho takatifu ilikuwa ikimsihi kupatana na sala zilizoongozwa kwa roho zilizomo ndani ya Biblia. Huenda ikawa kwamba yeye huzijibu katika njia ile ile aliyojibu sala hizo zamani, katika nyakati za Biblia.

8. Kwa hiyo roho inatusaidiaje udhaifu wetu, na kufanikiwaje?

8 Kwa kuwa roho takatifu iliongoza kuandikwa kwa sala hizo za kwanza ambazo katika hizo Mungu anasihiwa, inaweza kusemwa kwamba roho “huwaombea watakatifu kama apendavyo Mungu.” Katika njia hii ‘roho nayo hutusaidia udhaifu wetu.’ (Rum. 8:26, 27) Mungu hakosi kuitikia kusihiwa huko anakosihiwa na roho yake takatifu ikiwa mwombezi.

9. Tunaona nini kuhusu yale yanayosemwa katika sala zilizoandikwa katika Biblia, na ni kwa sababu gani “kuugua usikoweza kutamkwa” kwetu si kwa bure?

9 Kwa hiyo si ajabu kwamba, ikiwa Wakristo wangechunguza sala zilizoongozwa kwa roho ambazo zimeandikwa katika Zaburi na katika sehemu nyinginezo za Maandiko Matakatifu, watapata sala zinazoeleza jinsi walivyojisikia hasa, sala zinazosema yale yale waliyotaka kumwomba Mungu hasa ama kwa ajili yao wenyewe mmoja mmoja ama kwa ajili yao wote kama kundi la Kikristo. Wanachochewa sana ndani ndani ya mioyo yao kwa kuzipata sala hizi zilizoongozwa kwa roho takatifu ziseme mambo yaliyofaa sana jinsi hiyo. ‘Kuugua kwao wenyewe kusikoweza kutamkwa’ hakukuwa kwa bure, hakukukosa kufahamika wala hakukutupiliwa mbali. Hivyo kutoka kwa Maandiko yaliyoongozwa kwa roho wanakuja kujua maneno yaliyo dhahiri ambayo “roho” ilitumia kuwaombea mbele za Mungu. Wao wenyewe wanatiwa moyo na uhakika ulioonyeshwa na mtume Paulo aendeleapo kusema: “Sasa twajua kwamba Mungu hufanya kazi zake zote zishirikiane kwa faida ya wale wampendao Mungu.”​—Rum. 8:28, NW.

10, 11. (a) Ni nguvu gani inayotenda kazi kwa nguvu sana kama vile Mungu aendeleavyo kufanya kazi zake zote zishirikiane pamoja kwa faida za wale wampendao? (b) Ni kukombolewa kupi kunakokaribia kwa ajili ya ‘‘kiumbe kipya,” nako kwamaanisha nini vile-vile kwa wanadamu wanaougua?

10 Roho takatifu ya Mungu hutenda kwa nguvu sana katika kushirikiana na kazi zote za Mungu kwa faida za wale wampendao Mungu. Lo! namna hii nguvu ya utendaji takatifu ilivyo mpango wa ajabu wa Mungu! Roho ya Mungu inayojieleza kwa nguvu sana katika Biblia iliyoongozwa kwa roho, inaleta matokeo zaidi sana kuliko gurudumu lo lote la sala la wapagani au kitabu cho chote cha sala kilichotungwa na viongozi wa dini wa Jumuiya ya Wakristo kiwe kikisomwa katika nyakati na hali za pekee au kwa watu wa pekee.

11 Kuumba kwa kale sana kwa kibinadamu hakuna roho hii, na katika karne hii ya 20 kunaugua hata zaidi kuliko wakati mwingine wo wote uliotangulia, kukitafuta kukombolewa kwa njia yo yote kutokana na utumwa wa uharibifu wa taratibu ya mambo ya kale. Walakini karne 19 zilizopita, “kiumbe kipya” cha Mungu kilipata kuzaliwa na kuanza kutenda. Kilifanya hivyo chini ya uwezo wenye kutoa nguvu wa roho takatifu ya Mungu, iliyoanza kumiminwa katika siku yenye sherehe ya Pentekoste ya mwaka 33 W.K. Jitihada za kuumba kwa kale kwa kibinadamu katika kukiharibu “kiumbe kipya” cha Mungu, kundi la Kikristo lililozaliwa kwa roho, zimekuwa za bure. Leo hicho “kiumbe kipya” kinakaribia kukombolewa kwacho kutoka kwa mwili wacho wa kidunia uharibikao. Kukaribia kwa kukombolewa kwacho kwenye utukufu kunamaanisha mema kwa wanadamu wote. Kunamaanisha kwamba vilevile kukombolewa kwa wanadamu wanaougua kunakaribia. Kunamaanisha kwamba sasa inakaribia taratibu mpya yenye haki inayotegemezwa na roho takatifu ya Mungu.

—Kutoka Holy Spirit—The Force Behind the Coming New Order, Sura ya saba.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki