Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w81 1/15 uku. 24
  • Namna Magumu ya Ndoa Yao Yalivyomalizwa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Namna Magumu ya Ndoa Yao Yalivyomalizwa
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
w81 1/15 uku. 24

Namna Magumu ya Ndoa Yao Yalivyomalizwa

Magumu ya ndoa yanawapata mamilioni leo. Mara nyingi yanayosababisha magumu hayo ni matendo yasiyo ya kufikiria au hata ya kijeuri ya mwenzi mmoja au yule mwingine. Walakini watu wengi wamepata kutatua magumu ya ndoa yao. Kwa mfano, ebu angalia namna jambo hilo lilivyotukia kwa habari ya mume na mke katika sehemu ya mashariki ya Ulaya.

Kwa muda wa miaka mingi, Stefen alikuwa akilewa pombe mara nyingi, akampiga kinyama mke wake na kutumia vibaya fedha zake kwa kucheza kamari kwenye mbio za farasi. Yajapokuwa magumu aliyovumilia mke wake wakati huo, yeye aliendelea kuishi pamoja naye na kumpa msaada wa kifedha. Ndipo Stefen alipoanza kujifunza Biblia na mwishowe akawa mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Ijapokuwa alikuwa amebadili njia yake yote ya maisha ikawa bora zaidi, mke wake alitafuta kumtaliki wakati huo.​—1 Kor. 6:9-11.

Kortini, wakati hakimu alipouliza sababu fulani za talaka hiyo, mwanamke huyo hakuweza kusema lo lote baya kuhusu mwenendo wa wakati huo wa mume wake. Kwa hiyo, ndoa hiyo haikuvunjwa. Baada ya muda kupita, mwanamke huyo aliufungua moyo wake ukubali kweli na baada ya kujifunza Biblia kwa muda wa miezi minane alionyesha wakf wake kwa Mungu kwa kubatizwa katika maji. Leo, mume na mke hao wanapata furaha katika kumwabudu pamoja Yehova, Mungu wa rehema.

Kanuni za Ukristo zikitumiwa huwafanya waume, wake na watoto kuwa bora zaidi. Nayo Biblia inatoa msaada katika kutatua magumu. Inawapa vilevile wale wanaoukubali ujumbe wake tumaini la kweli na lenye uzima linalowaletea furaha.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki