Msaada Usiotazamiwa
SHAHIDI mmoja wa Yehova katika Newfoundland alipoteza kazi yake ya kuwa mjenzi. Vilevile, watoto wake, mmoja wa miaka minne na mwingine wa miaka sita, walihitaji matibabu ya namna ya pekee kwa sababu ya kufura zaidi kwa mfuko wa mkojo. Hata hivyo jamaa hiyo ilijikaza ikataka sana kuhudhuria kusanyiko la Kikristo katika Montreal, Quebec, Canada.
KWA KUWA ilielekea kwamba jamaa hii isingeweza kulihudhuria kusanyiko, baba alianza kuwasaidia watu wengine waweze kuhudhuria. Lakini yeye mwenyewe hakuacha hamu yake ya kutaka kuwa kusanyikoni.
KARIBU juma moja hivi kabla ya kusanyiko, Shahidi huyu alijiuliza hivi akishangaa: “Je! naweza kutega samaki-salmoni watakaotosha kulipia nauli ya kwenda?” Ilikuwa vigumu sana kufanikiwa katika jambo hilo kwa sababu ni samaki wachache sana wa namna hiyo waliovuliwa katika eneo hilo. Kama mtu fulani aliweza kuwavua, alivua mmoja tu kwa muda wa juma mbili au tatu. Isitoshe, Shahidi huyu hakuwa na leseni (kibali ya kisheria) ya kuvulia samaki.
BILA KUVUNJIKA MOYO Shahidi alifanya mipango ya kujipatia leseni ya kuvulia samaki kisha akatega wavu wake. Ajabu ni kwamba katika muda wa siku chache alivua samaki-salmoni wazuri 22. Mmoja wao alikuwa mkubwa sana hata akaweza kumwuza dola 34 (shilingi 340.00).
MATATIZO mengine yalitatuliwa na jamaa ikaweza kulihudhuria kusanyiko. Haijulikani kama Shahidi huyu alikuwa au hakuwa amewaza juu ya samaki wengi waliovuliwa chini ya usimamizi wa Yesu Kristo. (Luka 5:4-9) Hata hivyo, mwanamume huyu Mkristo alisadiki kwamba Mungu alizibariki jitihada zake.
JE! WEWE unapanga kulihudhuria “Kweli ya Ufalme” Kusanyiko la Wilaya la Mashahidi wa Yehova linalokuja? Je! kuna matatizo fulani yanayokuzuia? Basi, sababu gani usimwombe sana Yehova Mungu akusaidie? Mkono wake si mfupi, nawe huenda ukafurahia kupata msaada usiotazamiwa utakaokuwezesha ulihudhurie kusanyiko hilo la Kikristo lenye thawabu za kiroho.—Isaya 59:1.