Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w81 5/15 uku. 24
  • Sala na Jitihada Zathawabishwa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sala na Jitihada Zathawabishwa
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
w81 5/15 uku. 24

Sala na Jitihada Zathawabishwa

MTUME Mkristo Paulo aliwasihi waamini wenzake ‘wadumu katika sala.’ (Rum. 12:12, NW) Naye alifanya hivyo akiwa na sababu nzuri, kwa kuwa Paulo alijua kwamba sala ya namna hiyo inaleta faida. Mungu anajibu sala zinazofaa zinazopatana na mapenzi ya kimungu. Bila shaka, mara nyingi, lazima jitihada yenye bidii iambatane na sala yenye bidii. Kutoa mfano:

Katika mashamba makubwa ya ndizi huko Ecuador kulikuwako kikundi kidogo cha wahubiri 10 hivi wa ufalme wa Mungu. Ilikuwa lazima watembee kwa miguu kwa saa nyingi ili wafike kwenye mikutano ya Kikristo, nayo maeneo yao ya kutolea ushuhuda yalitapakaa sana hata kwamba iliwachukua saa mbili au tatu ili wawafikie jirani zao wakienda kwa miguu. Lakini mashahidi hawa wa Yehova wamethawabishwa kwa sababu ya jitihada yao katika kutangaza, au kujulisha, “habari njema.”​—Isa. 52:7.

Shahidi mmoja katika eneo hilo—mwanamume wa miaka 60—alisali kwamba Yehova Mungu ambariki kwa kumwezesha apate na kuongoza funzo la Biblia pamoja na mtu mwenye kupendezwa. Upesi akawa akiongoza funzo moja. Hata hivyo, mtangazaji huyu wa Ufalme, aliendelea kusali kwamba Mungu ambariki zaidi ili kwamba kwenda kwake kwa miguu kwenye eneo hilo kusiwe bure. Matokeo yakawaje? Kwani, upesi akawa akiongoza mafunzo manne mbalimbali ya Biblia pamoja na watu mmoja mmoja waliokuwa wakionyesha kupendezwa na “habari njema”!

Jitihada za watangazaji hao 10 wa Ufalme zimebarikiwa vilevile. Ilionekana kuwa hivyo wakati walipoweza kuwaleta pamoja watu 80 kwenye hotuba ya watu wote wakati wa ziara ya mwangalizi asafiriye. Watu fulani mmoja mmoja waliohudhuria walikuwa wametembea kwa miguu kwa muda wa saa nyingi ili waweze kuhudhuria.

Kwamba wako kwenye maeneo yaliyo peke yake au kwingineko, Mashahidi wa Yehova wanafurahia kushiriki pamoja na wengine “habari njema za Mungu wa furaha.” (1Tim. 1:11, NW) Katika utendaji huu mara nyingi sala zao za unyofu pamoja na jitihada zenye bidii zinathawabishwa. Kwa sababu gani usizungumze Biblia pamoja na Mashahidi wakutembeleapo tena nyumbani kwako? Kufanya hivyo kwaweza kukuthawabisha wewe kiroho.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki