Namna Walivyopata Maisha ya Jamaa Yenye Furaha
MIAKA kadha iliyopita Mashahidi wa Yehova wawili—wenzi wawili waliooana walio katika utumishi wa wakati wote katika utendaji wa kuhubiri wakiwa mapainia wa pekee—walikutana na jamaa yenye urafiki kutoka Czechoslovakia waliokuwa wakiishi katika Switzerland. Mke alikuwa mwalimu naye mumewe alikuwa mwana-michezo mwenye kutokeza sana katika mchezo wa mbio za mashua. Wote wawili walikuwa wamelelewa katika hali ya kuamini kutokuwako kwa Mungu, na iwapo Mungu angetajwa ama Biblia walikuwa wakidhihaki. Baada ya kuwa na mazungumzo nao kwa muda fulani, mapainia hao waliacha kuwatembelea.
Hata hivyo, baadaye, “Mnara wa Mlinzi” (Kiingereza) ulichapa makala juu ya mtu mweusi aliyekuwa amejipatia medali (nishani) ya dhahabu akiwa mpiga-mbio kwenye Michezo ya Olympic huko Tokyo (Japan). Huyo Shahidi (ambaye sasa alikuwa amefiwa na mumewe) anaandika hivi:
‘Nilikumbuka wenzi wale wawili wa kutoka Czechoslovakia, kwa sababu mume alikuwa amepata medali ya fedha katika Michezo iyo hiyo ya Olympic. Kwa hiyo makala hiyo ikawa ishara kwangu niitembelee jamaa hiyo tena. Kwanza, tulizungumza juu ya michezo mimi nikiwa msikilizaji tu. Katika ziara zilizofuata, nilisema tena na tena juu ya Biblia. Lakini mara nyingi nilikatizwa kwa maneno haya: “Tafadhali, Bi.——. Umesahau kwamba sisi hatuamini kuwako kwa Mungu.” Hata hivyo, niliendelea kuitembelea jamaa hii nzuri sana. Kitu fulani kilikuwa kikiniambia kwamba mambo yote hayakuwa sawa.
‘Mwishowe, nilipata kuona kwamba walikuwa na matatizo ya kijamaa. Tayari walikuwa wakisema juu ya kutalikana. Kwa hiyo nikawaonyesha kutokana na Biblia namna ya kushinda matatizo ya namna hiyo. Wenzi hao wawili walishangaa sana kuona shauri hilo lenye kufaa sana linalopatikana katika Maandiko nao wakakubali kujifunza Biblia. Ndoa yao kutiwa nguvu nao wakazamishwa katika kusanyiko moja la mzunguko.’
Kwa kuzamishwa katika maji, au kubatizwa, wenzi hao wawili wakaonyesha wakf wao kwa Mungu. Akikumbuka mambo ya kiroho yenye kufaa yaliyokuwa yametukia maishani mwao, mwanamume huyo alisema hivi:
“Wakati uliopita, singevumilia kusikia maneno kama vile ‘-takatifu,’ ‘malaika’ na maneno mengine kama hayo. Yalikuwa yakiumiza masikio yangu. Vilevile sikutaka kusikia jambo lote kuhusu mikutano. Lakini sasa kila kitu kimebadilika. Sasa saa zangu [za ziada] ni za Mungu na jamaa yangu. Vilevile, tumefanya mabadiliko kwa habari ya rafiki. Na sasa najua jinsi mikutano ya Kikristo ilivyo ya maana sana. Zaidi ya hayo, nimejifunza kuchukua daraka langu kama baba, nasi sasa tuna maisha ya jamaa yenye furaha. Nataka kumshukuru Yehova Mungu tena kwa sababu tuliruhusiwa kujifunza kusali na kwamba alitusaidia kabla ya sisi kumtafuta.”
Wengine, pia, wamesaidiwa na kitabu “Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha.” Sura zinatia ndani “Kuona Njia ya Kupata Furaha ya Jamaa,” “Kuendelea Kupashana Habari” na nyinginezo. Pokea kitabu hiki chenye thamani cha kurasa 192, bila malipo ya posta, kwa kupeleka shilingi 5.00 (1Z) kwa International Bible Students Association, Box 47788, Nairobi, Kenya; Mashahidi wa Yehova, B. P. 634, Limete-Kinshasa, Rep. Du Zaire.