Kiliwasaidia Waache Kuvuta Sigara
Mwanafunzi mmoja kijana huko Ubelgiji aliacha kuvuta sigara. Nafasi ilipopatikana, aliwaeleza wanashule wenzake sababu ya kuacha. Aliwaonyesha mambo yanayosemwa juu yake katika kitabu Kupata Faida Zote za Ujana Wako, akawaangushia nakala za kitabu hicho.
Mmojawapo wa wanafunzi hao aliacha kuvuta sigara baada ya kusoma kitabu hicho. Mama ya mwanafunzi mwingine alisoma kitabu hicho, naye akamkataza mwanawe asiendelee kuvuta sigara. Mama mwingine aliomba vitabu zaidi. Msimamizi wa shule hiyo alivutwa na yaliyokuwa yakitokea, naye pia akapendezwa na vitabu vya Mashahidi wa Yehova. Kwa ujumla, vitabu 30 viligawanywa.
Zaidi ya kuzungumza juu ya uvutaji wa sigara, kitabu hicho kinazungumza juu ya matumizi ya dawa za kulevya na vileo, na mambo mengine mengi yanayowapata vijana, kutia michezo, muziki, kucheza dansi, matembezi ya wavulana na wasichana na kuchumbiana. Pokea nakala kwa kujaza na kupeleka kisehemu hiki cha karatasi kilicho chini.
Tafadhalini nileteeni, bila malipo ya posta, kitabu chenye jalada ngumu cha kurasa 192 “Kupata Faida Zote za Ujana Wako.” Nimewapelekeeni shilingi 5.00 (ZI).