Kwa Maarifa ya Msingi ya Biblia
Kitabu chenye picha nzuri sana kinachoitwa Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia kinaeleza habari za Biblia kwa njia ya kupendeza sana na iliyo nyepesi kufahamika. Tayari nakala zaidi ya milioni 15 zimekwisha kupigwa chapa tangu kitolewe mwaka wa 1978. Barua inayofuata liliyoandikiwa afisi ya tawi la Ghana (Afrika) ya Sosaiti inaonyesha namna watu wamekuwa wakikiomba:
“Wapendwa-Katika-Kristo,
“MAOMBI YA KUNUNUA ‘KITABU CHANGU CHA HADITHI ZA BIBLIA’
“Nimefurahia sana kusoma nakala ya kitabu kinachoitwa ‘Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia,’ nilichoazimwa na rafiki yangu.
“Mimi naamini sana kwamba nikiwa na nakala yangu mwenyewe ya kitabu hicho kilicho kizuri sana, nitaweza kuwapa watoto wangu Neno la Mungu kwa wepesi na pia watoto wa nyumbani kwetu, ili wajipatie maarifa ya msingi juu ya Kristo.
‘Basi mimi nitamshukuru Mungu mkiweza kunipelekea nakala moja halafu mimi niwalipe baada ya hapo mkiisha kunieleza bei, au mnaweza kunielekeza nitakwenda wapi nikakinunue. Ningalikuwa nimetuma fedha kwa posta moja kwa moja lakini shida ni kwamba sijui bei ya kitabu chenyewe.
“Natazamia kwamba mtanisaidia katika jambo hili la haraka.
“Natazamia majibu yenu karibuni.
Wenu-Katika-Kristo,
E. O. A———.”
Ili wewe upokee nakala ya Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia, jaza tu hati yenye anwani iliyo hapa chini kisha uitume.
Tafadhalini nipelekeeni Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia, ambacho ni kitabu chenye ngozi ngumu cha kurasa 256, pamoja na kile kijitabu cha bure Wakati Ujao Salama—Jinsi Unavyoweza Kuuona. Mimi nimewapelekea shilingi 25.00