Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w81 7/15 uku. 4
  • Kutimizwa kwa Neno la Mungu ni Hakika

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kutimizwa kwa Neno la Mungu ni Hakika
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
w81 7/15 uku. 4

Kutimizwa kwa Neno la Mungu ni Hakika

Yehova Mungu alimwambia Ibrahimu hivi: “Kwa habari za Ishmaeli nimekusikia, nimembariki, nitamzidisha, nami nitamwongeza sana sana. Atazaa [wakuu] kumi na wawili, nami nitamfanya awe taifa kuu.” (Mwa. 17:20) Wakati huo Ishmaeli mwana wa Ibrahimu alikuwa mwenye umri wa miaka 13. (Mwa. 16:16; 17:1) Hakuna mwanadamu ye yote ambaye angeweza kutabiri kwamba kijana huyo aliyekuwa bado kuoa angekuwa baba ya wakuu 12. Walakini Muumba mwenye hekima yote alitabiri. Vyanzo viwili vya kihistoria vimehifadhi utimizo wa ufunuo huo wa kimungu, vikitaja wakuu 12 wafuatao: Nebayothi, Kedari, Abdeeli, Mibsamu, Mishma, Buma, Masa, Hadadi, Tema, Yeturi, Nafishi na Kedema. (Mwa. 25:13-15; 1 Nya. 1:29-31) Jambo hilo linaonyesha kwa nguvu uhakika wa kutimizwa kwa neno la kiunabii la Mungu!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki