Wewe Utakumbuka
Tarehe ilikuwa Nisani 14 ya mwaka wa 33 W.K. Yesu alikuwa akishiriki kunywa kikombe cha divai na kula mkate usiotiwa chachu pamoja na mitume wake. Aliwaagiza wafanye nini? “Endeleeni kufanya hivi katika kunikumbuka mimi.”—Luka 22:19, NW.
Kwa hiyo mara moja kwa mwaka Mashahidi wa Yehova kote kote ulimwenguni wanakusanyika kukumbuka kifo cha Yesu kwa njia aliyoagiza usiku ule alipotoa agizo hilo. Mwaka huu tarehe ya Nisani 14 itakuwa Machi 29. Wewe unakaribishwa kwa mikono miwili ujiunge nasi katika mkutano huu wa ukumbusho. Tafadhali waulize Mashahidi wa Yehova wanaokaa karibu nawe wakuambie wakati wa mkutano huu na mahali utakapofanyiwa.