Jambo la Thamani Kubwa Kuliko Kwenda Kanisani
Ni jambo gani hilo? Kulingana na mwanamume mmoja anayeishi Italia, ni kusoma gazeti Mnara wa Mlinzi. Yeye aliandika hivi:
“Mimi nilipokea zawadi ya uandikishaji wa gazeti lenu Mnara wa Mlinzi kutoka kwa mmoja wenu kisha nikawa nikisoma nakala za gazeti hilo mara tu zilipokuwa zikifika.
“Hakika lazima niwashukuru kwa sababu ya makala nzuri ajabu zilizo katika gazeti hilo. Ingawa habari zilizomo ni za kindani, zimeelezwa waziwazi na, zaidi ya yote, waandikaji wanaandika mambo yanayopatana kabisa na maandishi ya Biblia.
“Ingawa wakati mmoja nilikuwa nikitaja-taja sala tu kwa kumwomba Muumba wangu mara nilipoamka asubuhi, sasa mimi nasoma moja ya makala zilizo katika gazeti lenu kisha nayatafakari yaliyomo.
“Mimi ni mkulima wa kishamba kidogo na ninaishi peke yangu. Lakini tangu nilipowajua Mashahidi wa Yehova inaonekana nina marafiki wengi sana. Wanapokuja kutoka Asti kunitembelea inakuwa sawa na kutembelewa na mitume. Nakubali wazi kwamba nimejifunza mengi juu ya Biblia miezi michache iliyopita kuliko yale niliyojifunza muda wa miaka hamsini niliyokuwa nikienda kanisani.”
Ikiwa wewe ungependa kujifunza mengi zaidi juu ya mafundisho ya Biblia, tuna uhakika kwamba utalithamini gazeti Mnara wa Mlinzi. Unaweza kupelekewa nakala ishirini na nne kwa muda wa mwaka mmoja ukituma Kshs. 25/- (Tshs. 35/-, RWF 350) tu.
Tafadhalini mnipelekee Mnara wa Mlinzi. Nimewapelekea Kshs. 25/- (Tshs. 35/-, RWF 350). Lugha‐‐‐‐‐‐‐‐‐‐‐‐