Tukio Lililo la Maana Zaidi Katika Historia
Hilo lilikuwa tukio gani? Ni kifo cha Yesu Kristo. Kwa sababu gani?
Kwa sababu kifo chake kilisaidia kuondolea jina la Mungu malawama, kikahakikisha kwamba mwanadamu anaweza kuwa mkamilifu kuelekea Mungu akitaka.
Kifo hicho kilifungulia wanadamu taraja la kupata uzima wa milele katika hali za Paradiso.
Yesu mwenyewe alianzisha ukumbusho wa kifo chake usiku uliotangulia kufa kwake. Ukumbusho huo ulikuwa sherehe isiyo na mambo mengi. Wakati huo Yesu aliwaambia wanafunzi wake: “Endeleeni kufanya hivi katika kunikumbuka mimi.”—Luka 22:19, 20, NW.
Je! wewe utakumbuka?
Mashahidi wa Yehova wanakukaribisha ujiunge nao katika kuadhimisha tukio hilo lililo la maana zaidi katika historia. Mwaka huu tarehe ya kulikumbuka ni Jumapili, Aprili 15, baada ya jua kushuka. Unaweza kuhudhuria kwenye Jumba la Ufalme lililo karibu zaidi na nyumbani kwako. Hakuna pesa zitakazokusanywa, na wageni hawatatazamiwa wafanye lo lote isipokuwa kusikiliza hotuba yenye mafunzo na kujionea wenyewe namna mambo yatakavyoendeshwa bila sherehe nyingi. Waombe Mashahidi wa Yehova wa mahali unapokaa wakueleze wakati wenyewe hasa.