Chanzo cha Habari Yenye Kufaidi’
Hayo ndiyo maoni ya msomaji mmoja katika Koimbra, Ureno, kuhusu Amkeni! Anaandika hivi: “Ninachukua pindi hii kusema kwa mara nyingine ninavyothamini sana gazeti la Amkeni! Kusema kweli, ni zuri ajabu. Sikuzote ninalipokea kwa furaha ya roho na kulisoma sikuzote kwa uradhi mwingi na furaha ya kiroho. Sikuzote linatuletea makala nzuri, za mambo mbalimbali, yaliyoandikwa vizuri ili usomaji usiwe wenye kuchosha. Ninathamini gazeti hilo sana kwa ajili ya makala zalo, picha zalo, na mwishowe kwa ajili ya upendo ambao linatufanya tuwe nao kwa dunia na, kwa wazi, kwa Mungu. Ni kweli kwamba kuna mafundisho ya kidini nisiyokubaliana nayo, lakini ninasadiki kwamba roho iko pamoja na ninyi. Kwa habari ya elimu, naweza kusema tu kwamba Amkeni! linaelimisha sana na kulisoma ni chanzo kikubwa cha habari inayoongeza elimu ya ujumla ya mtu. Hongera! ”
Soma Amkeni! kwa ukawaida na ufurahie makala zalo zenye kupendeza na kuelimisha. Lipa Kshs. 28/- tu.
Tafadhali mnipelekee uandikishaji wa mwaka mzima wa Amkeni! Nimepeleka Kshs 28/- ili nipokee matoleo 12 ya magazeti hayo.