Usiku wa Kukumbukwa
Wakati wa sherehe isiyo na mambo mengi, Yesu Kristo alitumia divai na mkate usiotiwa chachu kuwa mifano ya dhabihu ambayo alikaribia kutoa kwa ajili ya wanadamu.
Alipokuwa akianzisha mwadhimisho huo, alisema: “Endeleeni kufanya hivi katika kunikumbuka mimi.”—Luka 22:19, NW.
Mwaka jana, watu 7,792,109 walimkumbuka Yesu kwa kuhudhuria ukumbusho wa kifo chake kwenye mikutano ya pekee iliyodhaminiwa ulimwenguni pote na Mashahidi wa Yehova. Unakaribishwa kwa moyo uhudhurie mwadhimisho wa Ukumbusho mwaka huu kwenye Jumba la Ufalme lililo karibu na nyumbani kwako.
Utafanywa Jumatatu, Machi 24, baada ya jua kushuka. Chunguza na Mashahidi wa Yehova wa kwenu ujue wakati barabara.