‘Kimenisaidia Niheshimiwe’
Hivyo ndivyo mwanamume mmoja wa Afrika Magharibi alivyosema kuhusu kitabu Kupata Faida Zote za Ujana Wako. “Mimi huita jamaa nzima mara nyingi ili tuwe na mazungumzo yanayokitegemea kitabu hiki,” ndivyo anavyoandika. “Vijana wa ujirani pia wanakuja kuyashiriki mazungumzo hayo. Shukrani kwa kitabu hicho, mimi nimeweza kuheshimiwa na vijana wote katika eneo letu nami nikawasaidia na matatizo yao.”
Kati ya yaliyo katika kichapo hiki chenye sura 24 ni mambo haya: “Waonaje Adabu?” “Je! Unywe Vileo?” “Nyimbo na Ngoma Unazochagua Kucheza,” “Je! Ni Busara Kutofanya Ngono Kabla ya Kufunga Ndoa?” na “Matembezi ya Wavulana Pamoja na Wasichana na Uchumba.” Unaweza kupata msaada huo mzuri sana wa kufanikisha maisha kwa kujaza na kutupelekea hati yenye anwani iliyopo chini pamoja na mchango wa Kshs. 15.00 tu (Tshs. 40.00).
Tafadhali mnipelekee, mkiwa mmelipia malipo ya posta, kile kitabu chenye jalada gumu cha kurasa 192 kinachoitwa Kupata Faida Zote za Ujana Wako. Mimi nimewapelekea Kshs. 15.00 (Tshs. 40.00).