Dalili ya Kuharibika kwa Maadili
WACHUNGUZI wa taabia za kijamii wanasema kuna mambo mbalimbali yanayofanya maadili yazidi kuharibika leo. Lakini, Cunningham Geikie mwanachuo wa Biblia wa karne ya 19, alionyesha kwa usahihi kabisa kile kinachopasa kulaumiwa. Yeye aliona upesi kwamba “ni ukweli wa daima kwamba tabia ya dini ya taifa ni dalili ya kuonyesha afya na nguvu zilizo katika taifa hilo.” Jambo la kupendeza ni kwamba, Biblia Takatifu inaonyesha dini ya uwongo ikiwa kama kahaba mwenye jina la kumtambulisha katika kipaji cha uso—‘Babuloni Mkuu.’ Katika mkono wake ana kikombe cha dhahabu kilichojawa na machukizo na machafu ya uasherati wake. Kwa wazi ni hali ya dini ya uwongo ya Kibabuloni iliyo dalili ya kweli ya kuonyesha ukosefu wa adili wenye madhara na uovu wa kushtusha uliopo leo.—Ufunuo 17:1, 2, 4, 5, 15.