Mbona Wanasema Mambo ya Kudharau-dharau?
Msomaji mmoja wa gazeti Amkeni! katika Uingereza alishindwa kujua ni kwa sababu gani watu wengine wanasema mambo ya kulidharau-dharau sana, akieleza hivi:
“Ingawa mimi si wa imani yenu, ninavutiwa daima na ufahamu mzuri na maelezo yenye kufahamika waziwazi yaliyo katika gazeti lenu.
“Mara nyingi nastaajabishwa na maneno ya kudharau-dharau yanayosemwa na wageni wanaonitembelea nyumbani wakati wanapoona nakala ikiwa imewekwa mahali fulani. Je! ingeweza kuwa ni kwa sababu gazeti Amkeni! linatueleza wazi sana mambo mengi ya kweli yanayotuhusu sisi wenyewe?
“Mwaka jana mimi nilipendezwa sana-sana na makala zenu juu ya uzoelevu wa kunywa pombe na, kwa kuwa hapo kwanza nilikuwa mlevi, kile kifungu kilichotolewa katika Biblia kuhusu kugeuka kwa kinywaji kuwa ‘kama nyoka’ kinanithibitishia mimi, kwa mara nyingine, hekima ya kitabu hicho.”
Wewe, pia, utavutiwa na Amkeni! Gazeti hili haligusi mambo juujuu tu, bali linayachunguza kwa ndani. Na kwa kuwa halisiti-siti kutaja mambo kwa kuogopa watangazaji wasiotaka yaelezwe wazi, linakuwa huru kutangaza mambo ya hakika. Wewe, pia, utafurahia gazeti hili, linalochapishwa katika lugha 53 na kusomwa na mamilioni ya watu.
Tafadhali mnipelekee andikisho la mwaka mmoja la Amkeni! Mimi nimewapelekea Kshs.28.00 (Tshs. 80.00) kwa matoleo 12 ya gazeti hili (nakala 1 kwa mwezi).