“Mvulana Wangu Hanipi Amani Hata Dakika Moja”
HIVYO ndivyo baba mmoja alivyoripoti alipokuja kwenye afisi ya tawi la Sosaiti yetu katika Peru hivi majuzi. Alieleza hivi:
“Mvulana wangu mdogo amekuwa akinisumbua-sumbua kwa majuma mengi, akitaka nimnunulie kile kitabu kinachoitwa Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia. Tangu wakati mmoja wa wanashule wenzake alipokipata, mvulana wangu hanipi amani hata dakika moja. Mimi nimekuwa nikiwaza sana ni wapi ningepata nakala moja. Sikujua hata kidogo ningeanzia wapi kutafuta. Nilipouliza kwenye maduka ya vitabu sikupata matokeo.
“Nilimtajia jambo hilo mmoja wa wafanya kazi afisini kwetu, naye akaniambia niendee Mashahidi wa Yehova nikakipate. Nikasema, ‘Ah, hapana! Siendi kwa watu hao. Wao wanakuja sikuzote mlangoni pangu, nami sikuzote nawaambia waende zao.’ Lakini yeye akanisadikisha kwamba ninyi si wabaya hivyo—kwa kweli, yeye aliwasifu sana ninyi na kusema kwamba kitabu ninachotafuta ni kizuri sana. Sasa nimekuja. Nataka kitabu hicho.”
Sisi tunaona kwamba wewe, pia, utakitaka kichapo hiki chenye picha za kupendeza sana, kilichoandikwa kwa herufi kubwa. Masimulizi yacho ya Kibiblia 116 yanampa msomaji wazo fulani ajue ni mambo gani hasa yaliyo katika Biblia.
Tafadhali mnipelekee, mkiwa mmelipia malipo ya posta, kile kichapo chenye jalada gumu kinachoitwa Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia. Mimi nimewapelekea Kshs. 35.00 (Tshs. 100.00).