Kushughulika na Hisia
Kushughulika na hisia zetu kwa mafanikio ni mwito wa ushindani kweli kweli. Kijana mmoja wa kike anaeleza jambo lililompata: “Mimi nilikuwa nikijihisi mwenye furaha, lakini dakika iliyofuata nikawa katika mshuko mkubwa wa moyo. Nyakati nyingine hata sikujua nilikuwa nikihisi nini. Ilikuwa kama kwamba nilikuwa nimepotea kabisa gizani. Sikuweza kueleza maoni yangu mwenyewe na jinsi nilivyoona moyoni hata kama nilisema na nani, hata sikuweza kujieleza mimi mwenyewe maoni niliyokuwa nayo. Nilihisi kama kwamba sikuwa nikielekezewa fikira na watu walionizunguka, hasa wanashule wenzangu, kwa sababu mimi sikuwa mwenye kuvutia vya kutosha. Hatimaye hisia zote zilikuwa zikinimaliza kwa ndani, nami nikaanza kujichukia mwenyewe na utu wangu.”
Msichana huyo alipata nakala ya kitabu Kupata Faida Zote za Ujana Wako. “Mambo yote ndani yalikuwa ya kupendeza sana,” msichana huyo aliandika, “kwa hiyo nikataka kusoma ile sura inayosema ‘Kuwa Mwanamke.’ Niliyokuwa nikisoma yaliniduwaza kwa sababu sura ile ilieleza mambo sawasawa na jinsi mimi nilivyokuwa nikihisi karibuni, na yakanipa jibu. Ilitia moyo sana kusoma kwamba ni jambo la kawaida kabisa watu kuhisi kwa njia hiyo. Ninalopaswa kufanya ni kujua tu njia inayofaa ya kushughulikia jambo hilo.”
Zaidi ya kusaidia vijana washughulike na hisia zao, kitabu hicho kinazungumza mambo kama vile kupiga punyeto, nacho kinatoa majibu kwa maulizo kama, Je! vijana wanywe vileo na, Je! wafanye ngono kabla ya ndoa? Wewe upokee nakala moja ya kitabu hicho kwa Kshs/ 15/- tu (Tshs. 45/-) kwa kujaza na kutupelekea hati yenye anwani iliyo hapa chini.
Tafadhali mnipelekee, mkiwa nimelipia malipo ya posta, kile kitabu chenye jalada gumu cha kurasa 192, Kupata Faida Zote za Ujana Wako Mimi nimewapelekea Kshs. 15/- (Tshs. 45/-).