Aliufikia Mradi Wake
Wakati wa hotuba ya Biblia, mhudumu mmoja alisema kwamba lazima Wakristo waweke miradi ya kibinafsi na kisha kujitahidi kuifikia. Msichana mwenye umri wa miaka minne ambaye alisikiliza hotuba hiyo aliwaambia wazazi wake asubuhi iliyofuata kwamba yeye alikuwa ameweka mradi wa kusikiliza Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia chote chenye kurasa 256 ambacho kimerekodiwa katika kanda. Mama yake anaandika hivi:
“Msichana huyo alijitayarisha mwenyewe kwa njia ya kustarehe akiwa na godoro, rekoda, kanda na kitabu, na akaomba kwamba apewe chakula chepesi wakati wa siku nzima. Nikifikiri ni mchezo tu, mimi nilikubali, nikifikiri kwamba angechoka kwa muda mfupi. Wakati wa asubuhi, nilimwangalia mara kadha kuona vile alivyokuwa akiendelea. Baada ya karibu saa mbili, mimi nilidokeza kwamba labda huo ulikuwa muda mrefu kutosha na kwamba tungeweza kumaliza kesho yake. Lakini yeye alikuwa ameazimia. Baadaye alasiri, yeye alitoka chumbani, akijinyoosha na akiwa anahisi mavune-vune kidogo, lakini akiwa na tabasamu yenye fahari. Ilikuwa imechukua karibu saa sita, lakini yeye alikuwa ameufikia mradi wake!
“Tangu wakati huo yeye ameanza shule, na mwalimu wake anasema kwamba yeye ndiye msomaji bora zaidi wa sauti kubwa ambaye wamepata kusikia.”
Wewe, pia, unaweza kupokea kanda hizi na Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia, au vyote viwili, kwa kujaza na kutupelekea hati yenye anwani iliyo hapa chini.
Tafadhali mnipelekee, mkiwa mmelipia malipo ya posta, ile pakiti ya rangi ya kahawia ikiwa na kanda nne ya Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia. Mimi nawapelekea Kshs. 150/- (Tshs. 420/-;). [ ] Mnipelekee Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia, chenye kurasa 256 zenye picha, nami ninawapelekea Kshs. 40/- (Tshs. 110;). [ ] Tia alama moja au zote, na kupeleka mchango ulio sahihi.