‘Nakala kwa Rafiki Zangu Binafsi’
Kwa sababu wamefurahia sana kitabu Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha, wengi wamewagawia wengine nakala. Kwa mfano, mtu fulani kutoka Indiana, U.S.A., anaandika hivi:
“Mimi ningependa kuwapongeza ninyi juu ya kitabu kizuri ajabu ambacho nimemaliza sasa hivi kukisoma, Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha. Ni kitabu ambacho kimeandikwa vizuri na kufahamika kwa urahisi, na vijana wetu na watu wa umri mkubwa pia wangenufaika kwa kukisoma.
“Mimi ningependa nakala zaidi kwa rafiki zangu binafsi, na ningependa pia kutumia kitabu hicho kama zawadi kwa watu wanaofanya arusi.
“Mimi ni wa imani ya Nazareti . . . na singefurahi vifaa vingine zaidi ya kitabu hicho, vipelekwe kwangu mimi . . . Ikiwa ingewezekana nipate kununua nakala kumi za kitabu hicho kwa bei nafuu, ningethamini kusikia kutoka kwenu.”
Pengine wewe unahisi juu ya kitabu Jamaa sawa na vile mtu huyo anavyohisi. Je! wewe unamjua mtu fulani ambaye ungependa ukishiriki naye? Sababu gani usimpelekee mtu huyo nakala ya zawadi? Unaweza kufanya hivyo kwa kujaza tu na kupeleka hati iliyopo chini, ukitia ndani pamoja na hati hiyo Kshs. 15/- (Tshs. 45/-).
Tafadhali pelekeni, mkiwa mmelipia malipo ya posta, kile kitabu chenye jalada gumu, chenye kurasa 192 Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha pamoja na barua ikieleza kwamba ni zawadi kutoka.
Mimi nimewapelekea Kshs. 15/- (Tshs. 45/-).