‘Watoto Wanakipenda Sana’
Mamilioni ya jamaa zimekifurahia Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia. Masimulizi yacho 116 ya Biblia yanampa msomaji wazo juu ya yale yaliyo katika Biblia. Mapema mwaka huu mwandikaji mmoja kutoka Australia Magharibi alieleza jinsi kitabu hicho ni chenye matokeo, akisema hivi:
“Mimi kazi yangu ni mwalimu nami natafuta kuwatia moyo watoto ninaowatunza wamtolee Mungu na Yesu kazi yao ya shule, kama vile mimi ninavyofanya katika kazi yangu kwa ajili ya watoto. Nimefanya uwe wajibu wangu kulisomea darasa ‘Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia’ chenu ambacho nilinunua kutoka kwa mmoja wa Mashahidi wenu wenye kuzuru. Watoto wanapenda kitabu, hadithi zilizomo, nao wananiomba niwasomee zaidi ninapokiweka kitabu chini.”
Je! kuna watoto unaojua ambao wangefurahia pia kukisoma Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia?Unaweza kupokea nakala moja kwa kujaza na kutupelekea hati yenye anwani iliyopo chini. Kitabu hicho kina kurasa 256, kina ukubwa wa gazeti hili, nacho kimejaa picha kubwa zaidi ya 125, nyingi zazo zikiwa zenye rangi yenye kupendeza.
Tafadhali mnipelekee mkiwa mmelipia malipo ya posta, kile kitabu chenye jalada gumu kinachoitwa Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia, mimi nimewapelekea Kshs. 40/- (Tshs. 110/-).