‘Kama Mkate na Maji kwa Moyo’
Hivyo ndivyo mhudumu mmoja Mprotestanti kutoka Malaga, Hispania, alivyosema ndivyo magazeti Mnara wa Mlinzi na Amkeni! yalivyokuwa kwake. Yeye alieleza hivi:
“Mimi nimekuwa pasta Mprotestanti kwa miaka kadha, na mimi naweza kuhakikishia ninyi kwamba katika mafunzo yangu yote ya kitheolojia, mimi sijapata urahisi na uwazi wa maelezo kama ule ambao vichapo vyenu vinao. Kwangu mimi, Mashahidi wa Yehova ni watu wanaoweza kuvutia wengine; katika ulimwengu wenye unafiki, wao wanaishi kulingana na mambo ambayo wao wanaitikadi nayo. . . .
“Kwa sasa, kwa sababu ya matatizo ya kibinafsi, mimi siwezi kujifunza pamoja na ninyi kama vile ningependa, lakini asante kwa Mungu, mimi napokea magazeti yenu, na hayo ni ‘mkate’ na ‘maji’ kwa moyo wangu, ambao unahisi njaa na kiu kwa ajili ya Mungu anayeishi.”
Wewe pia unaweza kufikiwa na Mnara wa Mlinzi na gazeti andamani la hilo Amkeni! kwa kujaza na kutupelekea hati yenye anwani iliyopo chini.
Tafadhali mnipeiekee andikisho la mwaka mmoja kwa Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mimi nimewapelekea ninyi Kshs. 97/-; (Tshs. 360/-).