Kuvumilia Chini ya Mkazo Uletwao na Nguvu Zinazopita Zile za Kibinadamu
Je! wewe unahisi kwamba hilo ndilo jambo ambalo wewe unafanya?
Watu wengi wanahisi hivyo. Na wao wanasaidiwa kwa kujua jinsi wengine wanavyokabili matatizo. Kadi moja kutoka Greenville,Teksasi, iliyopelekwa kwa Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi, ilieleza hivi: “Mimi nathamini kweli kweli yale masimulizi ya maisha ya kweli ya watu wa Kikristo ambao wamevumilia taabu nyingi ili kuwa waaminifu. Ni mengi mambo yaliyoonwa ambayo mimi nimesoma huku machozi yakitiririka usoni pangu, kwa kuwa mimi ningeweza kuona kwamba Yehova yule Mungu wa kweli ndiye peke yake aliweza kuwakomboa kutoka tatanishi kama yale ambayo wao walikuwamo. Inanifanya mimi nizidi kuwa Mkristo mwenye unyenyekevu na shukrani wakati ninaposoma mambo ambayo wao walipitia, na hayo yamenisaidia kufofikiri mengi mno juu yangu mwenyewe au kutokuwa mwenye ubinafsi.”
Kitabu cha Mwaka 1988 cha Mashahidi wa Yehova kimejawa na mambo yaliyoonwa ya Wakristo waliosimama imara kwa ajili ya uadilifu wakati wa ile vita katika Korea na wakati wa ile miaka ya uvamizi-haramu katika Ailandi. Hicho Kitabu cha Mwaka kinaandaa pia usimulizi wa kihistoria juu ya utendaji wa Mashahidi wa Yehova katika Kosta Rika, na pia kinaonyesha hali iliyopo sasa ya kazi yao ya ulimwenguni pote.
Tafadhali mnipelekee, mkiwa mmelipia malipo ya posta, Kitabu cha Mwaka 1988 cha Mashahidi wa Yehova, Mimi nawapelekea Kshs. 16/-; (Tshs. 60/-).