Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 2/15 uku. 21
  • Kujua Yaliyo Katika Habari

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kujua Yaliyo Katika Habari
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • “Baba Yetu . . .”
  • Makanisa Katika Deni
  • Vitumbuizo Visivyofaa
  • Kanisa La Kweli na Msingi Wake
    Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele
  • Kuna Hatari Gani Kujihusisha Kidogo Tu na Mambo ya Mizungu?
    Amkeni!—2002
  • Ni Nani Chanzo Halisi cha Uchawi?
    Amkeni!—2011
  • Je, Tuhudhurie Mikutano ya Kikristo?
    Amkeni!—2001
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 2/15 uku. 21

Kujua Yaliyo Katika Habari

“Baba Yetu . . .”

“Wanawake katika sehemu zote a nchi wamekuwa wakiambia waabudu wenzao kwamba wanahisi wakisumbuka fikira kwa kutumia maneno ya kiume tu (‘Baba yetu uliye mbinguni’) katika shughuli zao za ibada,” inaripoti Minneapolis Star and Tribune. “Hiyo inawafanya wahisi wakiwa kama raia wa hali ya chini, wanawake hao wanasema, na wanahisi hawawezi kupatana vizuri na mungu aliye wa kiume.” Likiunga mkono suala hilo, baraza la usimamizi wa United Methodist Church katika Minneapolis, Minnesota, U.S.A., lilipiga kura ya kupendelea kwamba orodha mpya ya maneno itumiwe na waenda-kanisani wanapotaja rejezo linalohusu Mungu wakati wa sala, shughuli za ibada, na utendaji mwingine wa kanisa.

Baadhi ya maneno yaliyotayarishwa na baraza la kanisa ambayo hayaonyeshi hali ya kiume wala ya kike, ni “chanzo cha amani, chanzo cha rehema, mwenye uthibitifu na upendo, aliye imara ya uhai wetu, . . . aliye akili ya ulimwengu wote mzima, . . . aliye wa juu na mtakatifu.” Utumizi wa maneno hayo utatiwa moyo uwe badala ya vijina vinavyoonyesha hali ya kiume na pia mitajo kama vile Bwana, Mfalme, na Baba, ambavyo vinamhesabu Mungu kuwa mwenye hali ya kiume.

Hata hivyo, hakuna kanuni ya kukataa utumizi wa Kibiblia wa marejezo ya kiume kwa Mungu. Muda mfupi kabla ya kifo chake, Yesu, Mwana mzaliwa-pekee wa Mungu, alilitumia waziwazi lile neno la Kiaramu Abba, linalomaanisha “Baba,” alipokuwa akimpeiekea sala Yehova Mungu. (Marko 14:36) Vivyo hivyo, mtume Paulo alitumia neno hilo kutokeza wazo la uhusiano wa usiri ulio kati ya Wakristo wapakwa mafuta na Baba yao wa kimbingu, Yehova. (Warumi 8:15; Wagalatia 4:6) Basi, ikiwa Yesu alifundisha wanafunzi wake kusali wakisema, “Baba yetu uliye mbinguni,” je! haiwapasi Wakristo wote kufanya hivyo?​—Mathayo 6:9.

Makanisa Katika Deni

Baada ya mkutano wa maafisa wa kanisa la Dutch Reformed Church kaskazini mwa Transvaal, Afrika Kusini, iliripotiwa kwamba yale makundi 134 ya kanisa yalikuwa na deni la R13.890,000 (dola 6,667,000 za United States). Ikieleza juu ya tatizo hilo, tahariri moja katika karatasi-habari Beeld ya Afrikaans iliuliza hivi: “Hata hivyo, je! kasoro yenyewe nyakati nyingine haiwi na baraza la kanisa?” Karatasi-habari hiyo inaeleza hivi: “Mara nyingi inakuwa kwamba shemasi anakuja-kuja nyumba hii na hii kila mwezi kukusanya pesa, lakini inajulikana wazi sana kwamba yule mhudumu mwenyewe haonekani mara nyingi, na yule aliye mzee wa kanisa hajulikani hata kidogo katika eneo lake. Je! washiriki wa kanisa ndio wa kulaumiwa katika visa hivyo kwa sababu ya kupata wazo la kwamba kanisa linapendezwa na pesa zao tu, si na masilahi yao ya kiroho?”

Tofauti na hivyo, huduma ya Yesu na wanafunzi wake ilikazia upaji wa kiroho. (Mathayo 10:8) Ingawa mara nyingi wasikilizaji wenye kuthamini waliwasaidia kwa kujitolea kuwapa mahitaji ya msingi kama vile chakula na mahali pa kulala, wala Yesu wala wanafunzi wake hawakutafuta manufaa za kimwili, (Luka 10:5-9) Ni kama vile mtume Paulo alivyotaarifu: “Mimi nimekuwa sikutamani fedha wala dhahabu, wala mavazi ya mtu.” Badala ya hivyo, yeye aliwaonya kwa upole wahudumu wa kweli wa Mungu ‘waache namna yao ya maisha iwe bila upendo wa pesa.’ Ziara zake kutoka nyumba kwa nyumba zilifanywa ili yeye aweze ‘kutoa ushuhuda juu ya toba kuelekea Mungu na imani katika Bwana yetu Yesu.’ (Matendo 20:20, 21,33; Waebrania 13:5, NW) Viongozi wa kidini wa siku hiyo ndio walioelezwa na Luka mwandikaji wa Biblia kuwa wapenda pesa.”​—Luka 16:9-15, NW.

Vitumbuizo Visivyofaa

Kwa kusudi la kujifurahisha tu, wanafunzi Wajeremani katika Lahnstein walianza kutumia bilauri ya kunywea maji, wakiisogeza-sogeza kutoka herufi moja hadi herufi nyingine kwa “kuandika” ujumbe fulani ili wachochee roho wanaoongoza mafumbo ya ulimwengu wa roho. Tokeo lilikuwa nini?

“Watoto wa miaka kumi na mitano wanapayuka-payuka habari za mashetani wakiwa wamevurugika, wakiogopa kwenda chooni peke yao. Wakati wa usiku, watoto wanataka kulala pamoja na wazazi wao,” inaripoti karatasi-habari Rhein-Zeitung ya Ujeremani. Mbabaiko ulitokea miongoni mwa wengi wa wale ambao “wakiwa katika mikutano ya kimya kingi waliwaita roho na mwishowe wakamwita ‘Lusiferi.’” Akitoa elezo juu ya jinsi watoto walivyotenda “wakati ‘Lusiferi’ anaposemwa kuwa alipashana habari nao,” mwalimu mmoja alionelea hivi: “Hata watoto waliopatwa na bumbuazi kubwa zaidi walitulia sana kwa ghafula. Wao walipatwa na hofu kubwa.” Baada ya tukio hilo, kituo cha watoto cha mji huo kilikataza “michezo” hiyo, na wazazi waliombwa wasiwaache peke yao watoto wao walioingiwa na woga mwingi.

Kulingana na karatasi-habari hiyo, “wimbi la mafumbo ya ulimwengu wa roho limeanza kuingia katika sinema, TV, na sahani za santuri.” Hata hivyo, kuchezacheza katika mafumbo ya ulimwengu wa roho ili kujitumbuiza hakukuandalia wanafunzi Wajeremani wa Lahnstein ile raha waliyotazamia. Kwa sababu gani? Kwa sababu Biblia inatupa sisi habari ya kwamba Ibilisi ni mwenye ufundi na ‘anaongoza vibaya dunia yote inayokaliwa.’ Hiyo inayahusianisha matokeo ya utendaji wa Ibilisi duniani na “ole.” Shetani na ‘kani zake za roho zenye uovu’ (mashetani) anapasa kuonwa kwa uzito kuwa hatari halisi ya kiroho, na kuepukwa.​—Ufunuo 12:9, 12; Waefeso 6:11, 12; linganisha Matendo 19:19, NW

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki