Kukumbuka Kifo cha Yesu
Wakati wa sherehe isiyo na mapambo mengi, Yesu Kristo alitumia divai na mkate usiochachishwa ili viwe vifananisho vya uhai wa kibinadamu ambao yeye angedhabihu kwa ajili ya aina ya kibinadamu. Alipokuwa akianzisha sherehe hiyo, yeye alisema: “Endeleeni kufanya hivi katika kukumbuka mimi.”—Luka 22:19, NW.
Mwaka uliopita watu 8,965,221 walikumbuka Yesu kwa kuhudhuria Ukumbusho wa kifo chake kwenye mikutano ya pekee iliyodhaminiwa na Mashahidi wa Yehova. Wewe unaalikwa kwa uchangamfu uhudhurie mwadhimisho wa Ukumbusho mwaka huu kwenye Jumba la Ufalme lililo karibu zaidi na maskani yako. Huo utafanywa Ijumaa, Aprili 1, baada ya machweo ya jua. Chunguza na Mashahidi wa Yehova wa kwenu ili ujue wakati kamili.