Uzawa wa Yesu—Je! Ni Hekaya Tu?
ATI uzawa ya Kristo! Huo unadaiwa kuwa msingi wa sherehe kubwa sana ya kila mwaka ya Jumuiya ya Wakristo. Ingawaje, kwa kufikiri kuzuri, viongozi wengi wa kidini wanasukumia mbali pande mbalimbali za masimulizi ya Gospeli ya uzawa wa Yesu na kusema ni hekaya tu. Mathalani, The Interpreter’s Bible, inasema hivi juu ya simulizi la Mathayo juu ya ziara ya wanajimu, au “wanaume wenye hekima”: “Hivyo hakuna njia ya kuhakikisha kama imetiwa chumvi, au kweli kweli, kama ilipata kamwe ‘kutukia’ kama uhakika halisi. Thamani na maana ya masimulizi haya hayategemei usahihi wayo; badala yake hadithi hiyo ni ya kufikiriwa kama kazi ya sanaa.”
Wachambuzi hao mara nyingi wanabisha kwamba yale masimulizi ya Gospeli ya uzawa wa Kristo yanakosa habari zote ili yaonwe kuwa historia. Lakini katika kitabu chake The Life and Times of Jesus the Messiah, Alfred Edersheim anakanusha maneno hayo, akisema: “Huenda kwa usalama ikathibitishwa kwa maneno, ya kwamba hakuna masimulizi ya Maandiko yasiyokubalika au ya hekaya ya tukio hili la hekaya ambayo yangeweza kufafanuliwa kwa ukosefu huu wa habari au kutokuwapo kwazo. Kwa kuwa mambo mawili ya muhimu, sawa na yale ya (hekaya) au yale ya pokeo, ni kwamba kila mara wao wanatafuta kuwazunguka mashujaa wao kwa wingi wa utukufu, na kwamba wanajaribu kutoa habari, ambazo ni haba kwa sababu nyingine.”
Ijapokuwa hivyo, kwa sababu gani zile Gospeli zinatoa habari chache sana kuhusu uzawa wa Yesu? Sababu kuu ni kwamba kifo chake, ni cha maana kubwa zaidi wala si uzawa wake. (Mathayo 20:28) Edersheim anatukumbusha hivi zaidi: “Gospeli hazikukusudiwa kutoa maandishi ya maisha ya Yesu, wala hata habari zinazoyahusu; bali zilikuwa na makusudi haya mawili: kwamba wale ambao wanazisoma ‘wanaweza kuitikadi kwamba Yesu ni Kristo, Mwana wa Mungu,’ na kwa kuitikadi ‘wanaweza kupata uhai kupitia Jina Lake.’”