‘Zina Msaada wa Kuwa Miongozo kwa Maisha ya Kila Siku’
Hivyo ndivyo mwanamke mmoja kutoka Toronto, Kanada, alivyoita vichapo vya Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi Biblia na Trakti. “Mimi nafurahia kuvisoma na naona habari zenyewe kuwa zenye kuarifu sana, zenye kuchangamsha na juu ya yote, zina msaada wa kuwa miongozo kwa maisha ya kila siku.”
Mwanamke huyo aliongezea hivi: “Mimi ni mhitimu wa chuo kikuu, na ni lazima niwashtushe kwa kukiri kwamba mimi nimejifunza mengi zaidi kupitia vichapo vyenu kuliko vile nimejifunza kupitia miaka yangu yote ya masomo. Nilifurahia hasa kitabu chenu Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha. Hakuna vichapo vinginevyo vyote ambavyo vimeweza kusaidia sana maisha yangu kama vichapo vyenu—hivyo vimenisaidia kwa njia isiyo na kipimo; na kwa jambo hilo mimi nawapigia asante kweli kweli.
Kitabu kilichotajwa juu, Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha, kinatoa madokezo ya wazi yanayosaidia kutatua matatizo na kufanya ndoa iwe na upendezo ule ambao Muumba aliikusudia. Ili upate nakala yako, jaza na kutupelekea hati yenye anwani iliyopo chini, pamoja na mchango wa Kshs. 15.00 (Tshs. 80.00).
Tafadhali mnipelekee, mkiwa mmelipia malipo ya posta, kile kitabu chenye jalada gumu cha kurasa 192 Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha. Mimi nawapelekea Kshs. 15.00 (Tshs. 80.00).