Tukio la Kukumbuka!
Ilikuwa Nisani 14 ya mwaka 33 W.K.
Yesu alikuwa akishiriki kikombe cha divai na pande la mkate usiotiwa chachu pamoja na mitume wake. Agizo lake lilikuwa nini? “Endeleeni kufanya hivi katika kunikumbuka mimi.”—Luka 22:19; NW.
Kwa hiyo mara moja kwa mwaka Mashahidi wa Yehova kuzunguka ulimwengu hukusanyika kufanya ukumbusho wa kifo cha Yesu kwa njia aliyoagiza usiku aliotaarifu hivyo. Mwaka huu, Nisani 14 yaanza Jumatano, Machi 22, wakati wa jua kushuka. Wewe unaalikwa kwa mikono miwili ujiunge nasi katika mkutano huu wa ukumbusho jioni hiyo ya Jumatano. Tafadhali waulize Mashahidi wa Yehova wa kwenu wakati na mahali hususa pa mkutano huo.