Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w89 4/15 kur. 26-27
  • Tatanisho la Kikatoliki

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tatanisho la Kikatoliki
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Habari Zinazolingana
  • Mpinge Shetani, Naye Atakimbia!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Ibilisi—Si Ushirikina Tu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • ‘Mpinge Ibilisi’ Kama Yesu Alivyofanya
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Adui wa Uzima wa Milele
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
w89 4/15 kur. 26-27

Tatanisho la Kikatoliki

SASA hivi Kanisa Katoliki linakabili matatizo mawili kuhusiana na Ibilisi. Kwa upande mmoja, linalazimika kupigana na elekeo lililo miongoni mwa Wakatoliki wa ki-siku-hizi la kutilia shaka kuwako kwa Ibilisi. Kwa upande mwingine, linalazimika kushughulika na harakati isiyo rasmi ya kupunga pepo, au kuondoa roho waovu katika watu.

Papa John Paul wa 2 aliwakumbusha vijana Wakatoliki kwamba wanapaswa kumchukua Ibilisi kwa uzito. Katika barua moja, aliandika hivi: “Haiwapasi kuogopa kumtaja yule aliyekuwa wa kwanza kufanya ubaya kwa jina lake: yule Mwovu. Yeye ametumia na anaendelea kutumia mbinu za kutojifunua mwenyewe.”

Vilevile, kardinali Joseph Ratzinger, prifekti wa Kundi Takatifu la Fundisho la Imani, katika Roma, alitaarifu hivi: “Hata wanatheolojia wasio na utambuzi mwingi waseme nini, ibilisi, kwa kadiri ambavyo itikadi ya Kikristo inahusika, ni mtu wa kutatanisha lakini aliye halisi, mwenye utu wala si kitu cha ufananisho tu. Yeye ni uhalisi wenye nguvu nyingi.”

Kardinali Ratzinger alionyesha pia hangaiko kubwa juu ya mikutano inayofanywa na Wakatoliki katika nchi nyingi bila ruhusa ya kimamlaka. Katika barua ya tarehe ya Septemba 29, 1985, iliyoelekezwa kwa maaskofu wote Wakatoliki katika sehemu zote za ulimwengu, yeye aliandika hivi: “Kwa miaka kadhaa, katika mikutano fulani ya kikanisa, mikutano zaidi na zaidi ya sala inafanywa ili kukomboa watu katika uvutano wa kishetani.” Yeye aliwakumbusha maaskofu hao kwamba kulingana na sheria rasmi, hakuna mikutano yoyote ya jinsi hiyo inayopasa kufanywa bila ruhusa ya moja kwa moja kutoka askofu wa mahali panapohusika na kwamba ruhusa hiyo inapasa kupewa kwa mapadri peke yao. Hakuna mtu wa kikawaida aliye na haki ya kuyatamka “maneno ya kupunga pepo dhidi ya Shetani na malaika walioanguka.”

Nyusipepa ya kila siku ya Kifaransa, Le Figaro, iliripoti hivi: “‘Ongezeko kubwa’ la utendaji wa kupunga pepo na kupinga Shetani limetokea wazi muda wa miezi michache iliyopita katika Italia, hasa katika Turin, ambako kardinali Anastasio Ballestrero ametoka sasa tu kuwaweka wapunga-pepo wapya sita.” Ikionyesha kwamba jambo hilo ni la ulimwenguni pote, nyusipepa ya kila siku ya Paris, International Herald Tribune, iliandika hivi: “Kupendezwa kujua juu ya uwezekano wa kuwako kwa Shetani katika Turin ni sehemu moja tu ya zungumzio pana lililo ndani ya Kanisa Katoliki la Kiroma kuhusu ule uovu ambao hutajwa kuwa mtu kwa njia mbalimbali katika Andiko na fundisho la kanisa kwa kurejezewa kuwa ‘mkuu wa ulimwengu huu,’ ‘ile nguvu ya giza,’ ‘nyoka wa kale,’ ‘mchongezi.’”

Mshiriki wa Chuo cha Masomo Bora cha Kifaransa, Jean Dutourd, alitoa maelezo ya kupendeza juu ya mashaka ya ki-siku-hizi kuhusu kuwako kwa Shetani​—⁠yenye kusemwa hata na maaskofu Wakatoliki. Yeye aliandika hivi katika nyusipepa L’Est-Republicain ya Kifaransa: “Siku hizi kuamini Mungu ni kama hakufurahiwi, lakini kunavumiliwa tu. Hata hivyo, kuamini kwamba kuna Ibilisi kunaonwa kuwa jambo la mzaha kabisa. Mtajo wenyewe tu wa jina Shetani . . . huwachekesha sana watu wenye maarifa mengi, wenye vyeo vya juu kidogo katika jamii, wanasiasa, na pia, bila shaka, maaskofu wa hesabu kubwa vya kutosha. Kicheko chao kinanishangaza zaidi kwa sababu ingeelekea kuonekana kwamba Ibilisi amekuwa akielekeza fikira za pekee kwetu sisi tangu 1914.”

Ikiwa Wakatoliki, kutia na baadhi ya makasisi, wanahitaji kukumbushwa na papa na wengine kwamba Shetani yuko kweli kweli, je! hiyo haifanyiki kwa sababu kwa karne kadhaa kanisa limeweka mkazo mkubwa zaidi juu ya pokeo, falsafa, na nadharia zisizothibitishwa za kisayansi kuliko ule ambao limeweka juu ya Biblia?

Kutajwa kwa 1914 hapo juu kunafaa kweli kweli. Mwaka huo umetiwa alama katika unabii wa Biblia kuwa ndio ulioanza “siku za mwisho” wakati Ibilisi, akiwa “mtawala wa ulimwengu,” anafanya jitihada yake ya kufa au kupona ili kuangamiza aina ya binadamu wote. (2 Timotheo 3:1; Yohana 14:​30, NW) Kama vile tafsiri moja ya Biblia ya Kikatoliki inavyotaarifu, “Msiba unakuja​—⁠kwa sababu ibilisi amewashukia nyinyi chini akiwa na hasira inayowaka, akijua kwamba ana wakati kidogo uliobaki.” Ingefaa Wakatoliki wenye moyo mweupe wakubali ushuhuda wa Biblia. Kwa nini? Kwa sababu hali za ulimwengu leo zinathibitisha kwamba “ufalme wa Mungu u karibu.”​—⁠Ufunuo 12:7-12; Luka 21:​25-31, The New Jerusalem Bible.

Kwa kuwa Ufalme huo unaahidi kukomesha ukosefu wote wa uadilifu na visababishi vyao, kuondolewa kwa Ibilisi na wenye kumuunga mkono kumekaribia sana. Hata hivyo, watu wanaojua kwamba Ibilisi yuko ndio peke yao wanaoweza kusimama dhidi ya utawala wake na kutumainia kuokoka. Jinsi gani? Si kupitia upungaji wa pepo, bali, kama alivyoandika mtume Paulo, kwa kuvaa “suti kamili ya silaha kutoka kwa Mungu.” Ndiyo, Neno la Mungu linasema wazi: “Mpingeni Shetani, naye atawakimbia.” ​—⁠Waefeso 6:​11-18, NW; Yakobo 4:7.

[Picha katika ukurasa wa 26]

Ibilisi na roho waovu wake wametupwa chini kwenye ujirani wa dunia.​—⁠Ufunuo 12:​9, 12

[Hisani katika ukurasa wa 26]

Picture Book of Devils. Demons and Witchcraft/Ernst and Johanna Lehner/Dover

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki