“Huwezi Kupata Kitabu Kama Hiki Mahali Pengine Popote”
Hivyo ndivyo mwalimu wa shule katika Ohio, U.S.A., alivyosema alipokipokea kitabu “All Scripture Is Inspired of God and Beneficial.” Mwanafunzi wa kidato cha juu shuleni alikuwa amempa mwalimu huyo kitabu hicho kwa sababu mwalimu alikuwa ameomba habari fulani kuhusu Mashahidi wa Yehova, na mwanafunzi huyo alijua kwamba mwalimu huyo wa kike alifunza madarasa ya Biblia. Kijana huyo anaeleza hivi itikio la mwalimu wake alipokikubali kitabu:
“Alisisimuka. Alisema alikuwa amekuwa akitafuta kitabu kama hicho. Akanishukuru sana. Siku iliyofuata alisisimuka hata zaidi. Akanipa barua ndogo ya asante na akasema kwamba kitabu hicho kilikuwa bora kabisa. ‘Huwezi kupata kitabu kama hiki mahali pengine popote!’ akasema mwalimu huyo wa kike. ‘Kila jambo limepangwa vema sana. Nina hakika hiki kitathibitika kuwa chenye thamani kubwa katika madarasa yangu.’”
Kitabu “All Scripture Is Inspired of God and Beneflcial” hujibu mamia ya maswali kuhusu Biblia. Kina sura 78, kutia na moja inayohusu kila kimoja cha vitabu 66 vya Biblia. Ni cha jalada gumu; kurasa 352, ukubwa wacho ukiwa sawasawa na wa gazeti hili. Ni Kshs. 48/=.
Tafadhali mnipelekee, mkiwa mmelipia malipo ya posta, “All Scripture Is Inspired of God and Beneficial.” Mimi nawapelekea Kshs. 48/=.