Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w89 11/1 kur. 23-26
  • Mkusanyo Waleta Mshangilio Katika Japani

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mkusanyo Waleta Mshangilio Katika Japani
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Vichwa vidogo
  • Kuuweka Msingi
  • Ongezeko Kujapokuwako Taab Kubwa-Kubwa
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
w89 11/1 kur. 23-26

Mkusanyo Waleta Mshangilio Katika Japani

“ILIONEKANA wazi kwamba Wamisionari wale wanahisi mvunjiko-moyo wa kadiri kubwa.” Ndivyo alivyoonelea Charles T. Russell, msimamizi wa kwanza wa Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi Biblia na Trakti, baada ya uchunguzi wa kibinafsi aliofanya kuhusu hali ya kidini katika Japani katika 1912. Alikuwa akinena juu ya kushindwa kwa wamisionari wa Jumuiya ya Wakristo na akataarifu hivi: “Kile ambacho Wajapani wahitaji ni ‘Gospeli ya ufalme.’”

Je! uhitaji huu ungejazwa wakati wowote? Kianga cha ukweli kiliangazia Wajapani kupitia konzi moja tu la Mashahidi waaminifu wa Yehova katika miaka ya 1920 na 1930. Hata wakati wa Vita ya Ulimwengu 2, wachache walidumu katika kuvumisha habari njema ujapokuwako uonevu wa serikali ya kimilki. Hata hivyo, kazi pana zaidi ya kukusanya ilikuwa akibani kwa ajili ya mlolongo huu wa visiwa vilivyo katika Mashariki ya Mbali.

Wamisionari 15 wa Mnara wa Mlinzi walipofika katika 1949, Yehova alipuliza uhai mpya ukaingia ndani ya kazi ya kuhubiri Ufalme katika Japani. Wamisionari waliowasili karibuni waliona matokeo ya Vita ya Ulimwengu 2 kila mahali: Majiji yalikuwa mabomoko tu, na watu walivurugika, kwa maana mfumo wao wa kale wa thamani za kiadili ulikuwa umepinduliwa. Wamisionari wa Jumuiya ya Wakristo pia waliufanya upya utendaji wao katika Japani wakati ule ule, lakini wakashindwa kufanyiza Wakristo halisi kutokana na Wajapani. Wale wamisionari wa Mashahidi wa Yehova walio “mawasili wa 49” na wale zaidi ya 150 waliowafuata walikabili wito mkubwa sana wa ushindani kuhusu kupanda imani kuhusu Muumba, Yehova Mungu, katika akili na mioyo ya Wajapani. Walikabilije wito huu wa ushindani?

Kuuweka Msingi

Jitihada yao ya kimisionari ilianza kwenye nyumba ndogo ya ghorofa mbili katika Tokyo. Katika miaka ya 1950, mkusanyo ulikuja polepole. ‘Ni wachache tu watakaokuja katika ukweli katika Japani kabla ya Har–Magedoni,’ akawaza mmoja wa Wajapani wa kwanza kuziitikia habari njema katika siku hizo. Mmoja wa waangalizi wa mzunguko wa mapema akumbuka kukaza macho nje ya dirisha la garimoshi na kujiuliza kwa mshangao kama nyumba zilizo katika vijiji vidogo alivyovipita vingepata kufikiwa kwa habari njema.

Ilichukua karibu mwongo mmoja wa jitihada ya kimisionari ili hesabu ya wahubiri wa Ufalme katika Japani ifikie alama ya elfu moja. Lakini kufikia 1963, kwa sababu ya ongezeko lenye kuendelea-endelea kwa uthabiti, lile tawi hafifu la Tokyo lilibomolewa na jengo la saruji madhubuti la ghorofa sita likasimamishwa mahali palo.

Wamisionari waliweka msingi mzuri kwa ajili ya wakati ujao kwa kukaza kikiki roho ya upainia ndani ya mioyo ya wanafunzi wao wa Biblia. Yehova alibariki jitihada yenye muungamano ya wamisionari na mapainia Wajapani, na hesabu ya Mashahidi ikapanda ikafikia alama ya kumi elfu katika 1970. Katika 1972, ili kusonga mwendo mmoja na ongezeko lililokuwapo, matbaa ya ghorofa tatu na jengo la makao yenye ghorofa tano yalijengwa katika Numazu, kilometa 120 hivi kusini-magharibi mwa Tokyo. Sasa, badala ya kuchapiwa magazeti na kampuni ya nje, Mnara wa Mlinzi na Amkeni! yakawa yakitokezwa katika mashine ya tawi lenyewe la Japani ili kutumikia kazi ya kuhubiri Ufalme huko.

Ni nani angaliweza kutarajia kwamba kazi ya mkusanyo ingekua iwe kubwa kuliko vifaa vya Numazu katika muda wa miaka kumi ijayo? Lakini ikawa hivyo, na Yehova alikuwa ameweka akibani mpanuko zaidi wa ujenzi ili kushughulikia mavuno yenye kuongezeka.

Ongezeko Kujapokuwako Taab Kubwa-Kubwa

Jengo-tata la tawi jipya lenye ukubwa ulio mara tatu za lile lililokuwa katika Numazu lilimalizwa katika 1982 katika Ebina, kuelekea kidogo upande wa kusini wa Tokyo. Kufikia wakati lilipowekwa wakfu katika Mei wa mwaka huo, Yehova alikuwa amebariki Mashahidi katika Japani kwa vilele mfululizo vya wahubiri kwa zaidi ya miaka mitatu. Ongezeko hili liliendelea, na katika Mei 1985 hesabu ya wahubiri Wajapani ikafikia ile alama ya mia moja elfu. Ndiyo, Yehova alikuwa anaharakisha mwendo wa kazi katika wakati wayo yenyewe, kwa hiyo ikawa haiepukiki kuwa na mpanuko zaidi wa vifaa vya tawi. (Isaya 60:22) Miaka michache tu baada ya wakfu wa jengo-tata la kwanza la Ebina, Baraza Linaloongoza lilikubali kujengwa kwa kiwanda kipya cha ghorofa sita kikiwa na sakafu ya chini na kao lenye ghorofa nane.

Ushuhuda ulikuwa wazi kwamba Shetani hakufurahia ukuzi huu miongoni mwa watumishi wa Yehova kwa sababu mwezi ule wa baada ya kufikia ile alama ya wahubiri mia moja elfu, kesi nzito kuhusu kutiwa damu mishipani ilitokea katika Japani. Mvulana wa miaka kumi alikufa baada—lakini si kwa sababu—ya wazazi wake kukataa asitiwe damu mishipani. (Matendo 15:29) Tokeo ni kwamba, vyombo vya habari viliwaka moto dhidi ya Mashahidi. Ingawa wakati huo baba ya mvulana huyo hakuwa Shahidi aliyejiweka wakfu, yeye alivumilia kusumbuliwa sana na maneno ya waandishi wa habari. Baadaye alibatizwa na sasa anatumikia pamoja na mke wake akiwa painia wa kawaida.

Shambulio hili liliathirije kazi ya mkusanyo? Liliiathiri kidogo sana. Wanafunzi fulani wa Biblia waliacha mafunzo yao, lakini vilele vya wahubiri kila mwezi vikaendelea kuwapo bila kukoma, na Desemba 1988 ikatia alama miaka kumi ya vilele vya mfululizo. Wakati wa kile kipindi cha miaka saba kati ya wakfu wa jengo-tata la kwanza katika Ebina na wakfu wa lile jipya, hesabu ya wahubiri iliongezeka maradufu kutoka 67,000 ikawa zaidi ya 135,000, huku hesabu ya mapainia wa kawaida ikiwa mara tatu kutoka 12,000 hadi 36,000, na hesabu ya mafunzo ya nyumbani ya Biblia ikakaribia kuwa maradufu kutoka 97,000 hadi 172,000. Ni ushuhuda mzuri kama nini wa shangwe ya ushindi wa Yehova juu ya mashambulio ya Shetani juu ya watu wake!—Mithali 27:11.

[Picha katika ukurasa wa 24]

Kushoto: jengo jipya la kiwanda lililopo Ebina huku (chini kushoto) programu ya wakfu ikiendelea, na (chini kulia) sebule ya jengo jipya la makao

[Picha katika ukurasa wa 25]

Jengo jipya la makao na (sehemu ya ndani) maktaba ikiwa katika sakafu ya pili ya jengo la ofisi

[Picha katika ukurasa wa 26]

Wamisionari hawa 19 wa kutoka darasa la 11 la Gileadi walihudhuria wakfu. Utumishi wao wa wakati wote—kuongezea ule wa watano wengine wa kutoka darasa la 11 waliokufa wakiwa waaminifu katika mgawo wao Japani —wajumlika kuwa miaka 1,023

Washirika watatu wa Baraza Linaloongoza —Carey Barber, John Barr, na Lloyd Barry—walishiriki katika programu ya wakfu

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki