Faraja Katika Wakati wa Uhitaji
Barua inayofuata ilipokewa kutoka kwa mwanamume mmoja katika Baltimore, Maryland, U.S.A.: “Tafadhali mnipelekee kile kitabu chenye jalada gumu cha kurasa 192 na vielezi Je! Uzima Ndio Uu Huu Tu? Mimi ningependa kupata nakala mbili, kwa maana nataka kimoja kwa ajili ya rafiki. Niliona toleo hilo katika kikaratasi kiitwacho Kuna Tumaini Gani kwa Ajili ya Wapendwa Wafu? nilichopokea katika mlango wangu. Karibuni tu nimepoteza mpendwa aliyekuwa kipenzi kwangu kwa miaka 35, nami niliyaona maneno yaliyo katika kikaratasi hicho kuwa ya kupendeza na kufariji sana hivi kwamba sikutaka kukiharibu kwa kukata lile tangazo ambapo jina na anwani huwekwa. Asanteni kwa jitihada yenu yote. Kuanzia sasa na kuendelea nitahakikisha kusoma fasihi zote ambazo nyinyi huchapa.”
Kwa kufurahisha, kuna tumaini kwa ajili ya wapendwa wafu. Pokea uthibitisho wa kuchangamsha moyo katika kitabu Je! Uzima Ndio Uu Huu Tu? na pia ile trakti Kuna Tumaini Gani kwa Ajili ya Wapendwa Wafu? Jaza na utupelekee hati yenye anwani iliyoambatanishwa.
Mimi ningependa kupokea kile kitabu chenye jalada gumu cha kurasa 192 Je! Uzima Ndio Uu Huu Tu? na ile trakti Kuna Tumaini Gani kwa Ajili ya Wapendwa Wafu? Jaza na utupelekee hati yenye anwani iliyoambatanishwa.