Je! Wewe Ungefurahi Kupokea Ziara?
Mmoja wa Mashahidi wa Yehova angependa kukuzuru wewe na kukusaidia uongeze maarifa yako juu ya Mungu, Ufalme wake, na makusudi yake kama yalivyoandikwa katika Biblia. Sisi tuna uhakika kwamba habari hizi zitakusaidia, kwa maana zitatoa majibu yenye kutegemeka kwa matatizo ambayo sisi sote twayakabili leo. Mashahidi wa Yehova huandaa maagizo ya kibinafsi na ya kikundi katika Biblia bila malipo.
Kwa hiyo ikiwa wewe ungependa kupata ziara ya mtu mwenye kustahili katika nyumba yako, au mahali pengine pafaapo, sisi tutaterema kuipanga. Utasaidiwa upate si majibu tu kwa maswali yako ya Biblia bali pia majibu kwa matatizo yawezayo kutatuliwa kwa kutumia kanuni za Biblia. Ili ujipatie utumishi huu, jaza na upeleke hati yenye anwani iliyo hapa chini.