Maana ya Sala
“Katika Kiebrania, neno kuu la sala linatokana na shina, ‘kuhukumu,’ na namna ya kawaida ya kiwakilishi-nafsi kirejeshi . . . humaanisha kihalisi, ‘kujihukumu mwenyewe.’” Ndivyo kinavyoonelea The Authorised Daily Prayer Book. Maana yake ni kwamba kazi moja ya sala ni kwamba inapasa kusaidia mtu kuona kama anafikia viwango na matakwa ya uadilifu ya Mungu.
Kwa sababu hiyo, kotekote katika Biblia, tunaambiwa kwamba mtu asipokuwa anafanya mapenzi ya Mungu, sala zake hazitasikiwa kwa upendezi. “BWANA [Yehova, NW] yu mbali na wasio haki; bali husikia sala ya mwenye haki.”—Mithali 15:29; 1 Yohana 5:14.
Kujichunguza mbele ya Yehova Mungu kwa uhakika kwapasa kumfanya mtu anayesali awe mnyenyekevu na mwenye majuto. Hilo laongezea nguvu zaidi mfano wa maneno ya Yesu kuhusu Mfarisayo mwenye kujivuna na mtoza kodi mwenye majuto ambao walikuja kwenye hekalu wasali.—Luka 18:9-14.
Hivyo, iwe tunasali kwa Yehova ili kumshukuru, kumsifu, au kumwomba dua, sala sikuzote ni pindi ya kujichunguza. Katika njia hiyo, sala inatuvuta karibu na Yehova na kuimarisha uhusiano wetu pamoja naye.