Imani Yao Katika Mageuzi Ilidhoofishwa
Mwanamume kutoka Milwaukee, Wisconsin, U.S.A., aliandika mwaka jana kuonyesha uthamini wake “kwa kile kifaa kizuri ajabu kilichoandaliwa katika kitabu Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation?” Alieleza hivi:
“Miaka miwili iliyopita, nilikutana na wenzi wa ndoa kutoka Beijing, China, waliokuwa wakienda kwenye chuo cha utabibu huku Milwaukee. Walikuwa wastadi wa bayokemia, nao hawakuficha kwamba walikuwa na imani ya moyo mweupe katika mageuzi.
“Kwa uhakika walinipita kwa maarifa ya kisayansi nisiweze kuongea nao kisayansi, kwa hiyo niliamua kuacha kitabu kifundishe. Tulipoendelea na funzo letu, niliweza kuona uhakika wao katika mageuzi ukianza kuyumbayumba.”
Funzo la kitabu chote lilikamilishwa, na yule mwanamume kutoka Milwaukee amalizia hivi: “Biblia imekuwa kwao chanzo cha kweli cha habari. Asante tena kwa kifaa hicho kizuri ajabu.”
Ikiwa ungependa kupokea kitabu hicho cha kurasa 256 chenye vielezi vyenye kupendeza, tafadhali jaza na kupeleka hati-anwani hii yenye kuandama.
[Picha katika ukurasa wa 32]
Mbuni alihitajiwa kwa ajili ya kigumba hiki
Je! mbuni hakuhitajiwa kwa ajili ya chembe ya DNA? Ningependa kupokea kitabu Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation?