Je! Ungependa Kupokea Ziara?
Mwaka uliopita mwanamke mmoja kutoka Corpus Christi, Texas, U.S.A., aliandikia Watchtower Society katika Brooklyn, New York, akisema hivi: “Jina langu ni Emily, nami nimekuwa nikijifunza fasihi ambazo baadhi ya Mashahidi wa Yehova walinipa majuma machache yaliyopita. Baada ya kuyasoma magazeti na kuyalinganisha na Biblia yangu ya familia, niliona kwamba Kanisa Katoliki la Kiroma halikuonekana kama hufundisha yaliyokuwamo katika Biblia Takatifu. Wao hawakusema kamwe juu ya jina la Mungu wala juu ya Ufalme wa Mungu unaokuja, mambo ambayo niliyapata kuwa ndizo habari kuu katika Biblia yangu. Nimeacha kwenda kwenye kanisa la familia yetu na nimeanza kujifunza Biblia, kwa msaada wa fasihi zenu zenye kusema ukweli.
“Ningependa kuanza ushirika pamoja na kundi la kwetu la Mashahidi wa Yehova. Tafadhali wapelekeeni ujumbe waje nyumbani kwangu tupate kuongea.”
Mmoja wa Mashahidi wa Yehova angefurahi pia kukuzuru wewe na kukusaidia uongeze maarifa yako juu ya Mungu, Ufalme wake, na makusudi yake, kama yalivyoandikwa katika Biblia. Ili ujifaidi na utumishi huo, jaza tu habari ambazo zaombwa hapa chini na uzipeleke kwenye anwani iliyo katika hati yenye anwani.
Mimi ningependa kujua mengi zaidi juu ya Biblia. Tafadhali pangeni mtu fulani anitembelee.