Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w92 4/1 uku. 30
  • Dini ya ‘Imani Yenye Kubadilika-Badilika’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Dini ya ‘Imani Yenye Kubadilika-Badilika’
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
w92 4/1 uku. 30

Dini ya ‘Imani Yenye Kubadilika-Badilika’

“Uwezo wa Umormoni kujiimarisha katika demokrasia zenye uhuru zaidi na katika mataifa yenye utawala kamili ni ajabu kubwa.” Ndivyo lilivyoonelea jarida The Wall Street Journal wakati Hungari ilipolipa kanisa la Church of Jesus Christ of Latter-day Saints utambulisho kamili. Kanisa hilo linatimizaje hilo? “Ufunguo,” kulingana na Journal, “si kiwango cha Warmomoni cha juu cha kuzaa au kueneza injili yao kwa bidii tu. Bali, ni ubadilifu-badilifu ulioimarisha katika imani hiyo.” Jinsi gani hivyo?

Likinena juu ya kipindi kilichotangulia mabadiliko ya kisiasa ya karibuni katika Ulaya ya Mashariki, Journal lilisema hivi: “Wakitumia vikundi vya wapiga-muziki na wacheza-dansi za kitamaduni kutoka Brigham Young University, Wamormoni wamefaulu kuepuka vizuizi na ukosefu wa ushirikiano ambao wamishonari hukabili kwa ukawaida katika nchi nyingi za Kikomunisti,” lasema Journal. Vikundi vyao vya waimbaji vimekwenda Romania, Chekoslovakia, Hungary, Polandi, Urusi, na China, na vilevile hadi Saudi Arabia, Libya, Misri, Jordani, Somalia, na Israeli. Zaidi ya hilo, “utajiri wa Kanisa la Mormoni umetumiwa kuwa wenzo wa kupatia njia ya kuingia katika nchi za Kimarksisti na za Ulimwengu wa Tatu.” Ujenzi wa mabwawa na kuchimba visima ni miongoni mwa miradi inayotegemezwa na upaji wa Wamormoni.

Katika ulimwengu wa leo wenye kupenda anasa na wenye njaa ya pesa, haishangazi kwamba mbinu kama hizo za kuimba nyimbo, kucheza dansi na kutoa michango ya kifedha hutumiwa kupata waongofu. (2 Timotheo 3:2, 4) Lakini wenye mfano wa kondoo kweli kweli wanavutwa na sauti ya Mchungaji Mwema, Yesu Kristo. (Yohana 10:27) Ndiyo sababu, alipowaamuru wafuasi wake ‘wakafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote,’ yeye hakusema wakafanye hivyo kwa njia yoyote au kwa gharama yoyote bali kwa ‘kuwafundisha kuyashika mambo yote aliyokuwa amewaamuru.’ (Mathayo 28:19, 20) Katika kutimiza utume huu, hakuna nafasi ya kuridhiana kanuni za Biblia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki