Siku ya Kukumbukwa
Jioni ya kabla ya kufa kwake, Yesu alishiriki pamoja na mitume wake mkate usiotiwa chachu na kikombe cha divai, akasema: “Endeleeni kufanya hivi katika kunikumbuka mimi.”—Luka 22:19, NW. Mwaka huu mwadhimisho wa kila mwaka wa ombi lake utakuwa Aprili 1, baada ya jua kutua.
Kama tokeo, Mashahidi wa Yehova kuzunguka ulimwengu watakusanyika jioni hiyo ya pekee ili kurudia Ukumbusho huo kwa njia ile aliyoomba Yesu. Wakaribishwa kwa uchangamfu sana kukutana pamoja nasi. Tafadhali hakikisha pamoja na Mashahidi wa Yehova wa mahali unapoishi upate wakati na mahali barabara pa mkutano huo.