Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w92 12/1 uku. 32
  • “Kama Simba Angurumaye”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Kama Simba Angurumaye”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
w92 12/1 uku. 32

“Kama Simba Angurumaye”

JE! UNAAMINI kwamba Shetani yuko? Leo, wengi hawaamini. Yaonekana wao huona imani ya jinsi hiyo kutokuwa ya “kisayansi.” Hata huko nyuma katika 1911, Encyclopœdia Britannica ilisema hivi: “Sayansi imeeleza taratibu nyingi sana za asili ya nje na za maisha ya ndani ya mwanadamu hivi kwamba haiachii nafasi uwezo wa Kishetani.” Wanatheolojia husababu kwamba Shetani ni kifananisho tu, ngano. The World Book Encyclopedia hutaarifu hivi: “Wanatheolojia wengi wa ki-siku-hizi humwona Ibilisi kuwa kifananisho cha nguvu za uovu, au sifa mbaya zaidi ya asili ya kibinadamu.”

Lakini, ni mambo gani ya hakika? Ikiwa unaamini katika Biblia, ni lazima uamini kwamba Shetani ni halisi. Yesu hakuamini tu kwamba Shetani alikuwako bali pia alimwita “mkuu wa ulimwengu huu.” (Yohana 14:30) Mtume Paulo alimwita Shetani “mungu wa huu mfumo wa mambo.” (2 Wakorintho 4:4, NW) Na mtume Yohana aliyezeeka alisema hivi: “Ulimwengu mzima uko katika uwezo wa yule mwovu.”—1 Yohana 5:19.

Ikiwa hukubaliani na Yohana, fikiri juu ya historia ya hivi karibuni. Fikiri juu ya vikosi maalumu vya kuua na kutumiwa kwa mateso na serikali mbalimbali. Kumbuka vile vita na ule uuaji mwingi ambao kizazi chetu kimeona. Na namna gani uhalifu mkatili unaokuwa ndio kichwa kikuu cha magazeti yetu ya habari—uuaji wa matungamano ya watu, kulalwa kinguvu, mauaji ya mfululizo yanayofanywa na mtu mmoja mmoja, na kutendewa vibaya kigono kwa watoto, kutaja machache tu? Je! kuna yeyote mwingine ila Shetani ambaye ndiye mungu wa ulimwengu huu?

Mtume Mkristo Petro alionya hivi: “Mwe macho; kesheni! Maana adui yenu, Ibilisi, huzungukazunguka kama simba angurumaye akitafuta mawindo.” (1 Petro 5:8, HNWW) Ikiwa simba alikuwa huru katika ujirani mwako, je, ungekuwa ukizungumza juu ya kama alikuwako au la? Au ungekimbilia kificho?

Uwe na hakika kwamba Shetani yuko. Yeye hana rehema na ni mkatili, naye ana nguvu nyingi kuliko sisi. Kwa hiyo kimbia ili upate ulinzi kwa Yule ambaye ni mwenye nguvu hata zaidi. “Jina la BWANA [Yehova, NW] ni ngome imara; mwenye haki huikimbilia, akawa salama.” (Mithali 18:10) Pata himaya kwa Yehova Mungu, na ujue ya kwamba hivi karibuni ainabinadamu itawekwa huru na uvutano wa yule mwovu, Shetani. Hicho kitakuwa kitulizo chenye shangwe kama nini!—Ufunuo 20:1-3.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki