Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w93 11/1 kur. 30-31
  • Je! Wakristo wa mapema walitumia jina la Mungu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Wakristo wa mapema walitumia jina la Mungu?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
w93 11/1 kur. 30-31

Je! Wakristo wa mapema walitumia jina la Mungu?

JINA la Mungu hutokea mara maelfu katika Maandiko ya Kiebrania, ambamo linawakilishwa na zile konsonanti nne יהוה (YHWH, ile Tetragramatoni). Magunduzi ya kiakiolojia yadokeza kwamba katika Israeli wa kabla ya uhamisho, kabla ya 607 K.W.K., jina hilo lilitumiwa kikawaida, na katika vile vitabu vya Biblia vya baada ya uhamisho vya Ezra, Nehemia, Danieli, na Malaki, latokea mara nyingi. Lakini, polepole wakati wa kutokea kwa Mesiya ulipokaribia, Wayahudi walisita kulitumia jina hilo kwa sababu ya ushirikina.

Je! wanafunzi wa Yesu walitumia jina la Mungu (linalofasiriwa kwa kawaida kuwa “Yehova,” katika Kiswahili)? Ithibati yasema ndiyo. Yesu aliwafundisha wafuasi wake wasali kwa Mungu hivi: “Jina lako litukuzwe.” (Mathayo 6:9) Na mwishoni mwa huduma yake ya kidunia, yeye mwenyewe alisali kwa Baba yake wa kimbingu hivi: “Jina lako nimewadhihirishia watu wale ulionipa katika ulimwengu.” (Yohana 17:6) Zaidi ya hayo, nakala za mapema za Septuagint, tafsiri ya Kigiriki ya Maandiko ya Kiebrania iliyotumiwa na wanafunzi wa Yesu, zilikuwa na jina la Mungu kwa namna ya Tetragramatoni ya Kiebrania.

Namna gani zile Gospeli na sehemu nyinginezo za Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo (“Agano Jipya”)? Sababu imetolewa kwamba kwa kuwa jina la Mungu lilionekana katika Septuagint, lingeonekana pia katika nakala za mapema zaidi za Maandiko hayo—angalau mahali ambapo Septuagint ilinukuliwa. Hivyo, jina Yehova hutokea zaidi ya mara 200 katika New World Translation of the Christian Greek Scriptures. Wengine wamechambua hilo kuwa jambo lisilo haki. Hata hivyo, yaonekana kwamba New World Translation inaungwa mkono na chanzo kisichoelekea kufanya hivyo: Talmudi ya Babuloni.

Sehemu ya kwanza ya kitabu hicho cha kidini cha Kiyahudi ina kichwa Shabbath (Sabato) na ina mjumlisho wa amri nyingi sana zinazoongoza mwenendo wakati wa Sabato. Katika sehemu moja, kuna mazungumzo juu ya kama yafaa kuokoa hati-mkono za Biblia kutoka katika moto wakati wa Sabato, kisha fungu lifuatalo latokea: “Ilitaarifiwa katika maandishi-awali: Hatuwezi kuokoa kutoka katika moto, nafasi zilizo tupu [gil·yoh·nimʹ] na Vitabu vya Minim. R. Jose alisema hivi: Katika siku za juma ni lazima mtu akate Majina ya Kimungu yaliyo [katika hati-mkono], ayafiche, na kuchoma sehemu zile nyingine. R. Tarfon alisema: Na nipatwe na laana ya kumzika mwanangu kama nisingezichoma [hizo hati-mkono] pamoja na Majina yazo ya Kimungu iwapo ningezipata.”—Imetafsiriwa na Dakt. H. Freedman.

Mi·nimʹ walikuwa nani? Hilo neno lamaanisha “wanafarakano” na lingeweza kurejezea Masadukayo au Wasamaria. Lakini kulingana na Dakt. Freedman, yaelekea sana kwamba katika fungu hilo larejezea Wakristo Wayahudi. Kwa hiyo, gil·yoh·nimʹ, zilizotafsiriwa kuwa “nafasi zilizo tupu” kulingana na Dakt. Freedman, zilikuwa nini? Kuna maana mbili ziwezazo kuwa. Zingeweza kuwa pambizo za hati-kunjo au hata hati-kunjo zilizo tupu. Au—kwa kutumia neno hilo kinyume—zingeweza kuwa maandishi ya mi·nimʹ, kana kwamba ni kusema maandishi hayo hayafai kitu kama vile hati-kunjo zilizo tupu. Katika kamusi nyingi maana hiyo ya pili yatolewa kuwa “Gospeli.” Kwa kupatana na hilo, sentensi inayotokea katika Talmudi kabla ya sehemu iliyonukuliwa juu, yasomwa hivi: “Vitabu vya Minim ni kama nafasi zilizo tupu [gil·yoh·nimʹ].”

Kwa hiyo, katika kitabu Who Was a Jew? cha Lawrence H. Schiffman, sehemu ya Talmudi iliyonukuliwa juu inatafsiriwa ifuatavyo: “Hatuokoi kutoka katika moto (wakati wa Sabato) zile Gospeli na vitabu vya minim (‘wazushi’). Badala ya hivyo, vinachomwa mahali pavyo, hivyo pamoja na Tetragramata zavyo. Rabbi Yose Ha-Gelili asema hivi: Katika juma, mtu apaswa kukata Tetragramata zavyo na kuzificha na kuchoma masalio. Rabbi Tarfon alisema: Na nipatwe na laana ya kuwazika wana wangu! Ikiwa ningevipata (vitabu hivyo), ningevichoma pamoja na Tetragramata zavyo.” Dakt. Schiffman aendelea kutoa hoja kwamba mi·nimʹ hapa ni Wakristo Wayahudi.

Je! kweli sehemu hiyo ya Talmudi yasema juu ya Wakristo Wayahudi wa mapema? Ikiwa ndivyo, basi hiyo ni ithibati yenye nguvu kwamba Wakristo walitia ndani jina la Mungu, ile Tetragramatoni, katika Gospeli na maandishi yao. Na yaelekea sana kwamba hapa Talmudi inazungumzia Wayahudi Wakristo. Maoni hayo yana utegemezo wa kiusomi, na katika Talmudi muktadha waonekana kuwa watoa utegemezo zaidi. Sehemu inayofuata dondoo lililo juu kutoka katika Shabbath yasimulia hadithi inayohusisha Gamalieli na hakimu mmoja Mkristo ambayo katika hiyo sehemu za Mahubiri ya Mlimani yanatajwa.

Ni baadaye tu, wakati Ukristo wenye kuasi-imani ulipopotoka kutoka katika mafundisho sahili ya Yesu, kwamba jina la Mungu liliacha kutumiwa na wale waliodai kuwa Wakristo na hata likaondolewa kutoka katika nakala za Septuagint na kutoka katika zile Gospeli na vitabu vingine vya Biblia.

[Picha katika ukurasa wa 31]

Katika siku ya Yesu, jina la Mungu lilionekana katika “Septuagint”

[Hisani]

Israel Antiquities Authority

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki