Usiku wa Kukumbukwa
KATIKA siku yenye kukumbukwa zaidi ya miaka 3,500 iliyopita, Yehova Mungu aliwaamuru Waisraeli waliokuwa watumwa katika Misri, waue mwana-kondoo na kunyunyiza damu yayo juu ya miimo na vizingiti vya nyumba zao. Usiku uo huo, malaika wa Mungu alipita juu ya nyumba zilizotiwa alama kwa njia hiyo lakini akaua wana wazaliwa wa kwanza katika nyumba za Wamisri wote. Halafu Waisraeli wakaachiliwa huru. Tangu wakati huo, kwenye sherehe ya kukumbuka tukio hilo, Wayahudi wamesherehekea Sikukuu ya Kupitwa.
Mara tu baada ya Yesu Kristo kumaliza kusherehekea Sikukuu ya Kupitwa yake ya mwisho pamoja na mitume wake, yeye alianzisha mlo ambao ungekumbusha juu ya kifo chake cha kidhabihu. Yeye aliwapa mkate mitume wake waaminifu na kusema: “Twaeni, mle; huu ndio [wamaanisha, NW] mwili wangu.” Halafu akawapa kikombe cha divai na kusema: “Nyweni nyote katika hiki; kwa maana hii ndiyo [yamaanisha, NW] damu yangu ya agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi kwa ondoleo la dhambi.” Yesu pia alisema: “Fanyeni [endeleeni kufanya, NW] hivi kwa ukumbusho wangu.” (Mathayo 26:26-28; Luka 22:19, 20) Kwa hiyo Yesu aliwaamuru wafuasi wake wafanye mwadhimisho huo wa kifo chake.
Mashahidi wa Yehova wakualika kwa uchangamfu ujiunge nao katika kuadhimisha Ukumbusho huu wa kifo cha Yesu. Waweza kuhudhuria kwenye Jumba la Ufalme lililo karibu zaidi na nyumba yako. Chunguza na Mashahidi wa mahali unapoishi ili kujua wakati na mahali barabara. Tarehe ya mwadhimisho huo katika 1994 ni Jumamosi, Machi 26, mkate na divai ikipitishwa baada ya jua kushuka.