Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w94 5/1 kur. 3-4
  • Je! Dini Inatosheleza Mahitaji Yako?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Dini Inatosheleza Mahitaji Yako?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Habari Zinazolingana
  • Kitabu Cha Biblia Namba 5—Kumbukumbu La Torati
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • Kuzijua Njia za Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Musa—Jinsi Maisha Yake Yanavyokuhusu
    Amkeni!—2004
  • Yesu Kristo Alikuwaje Nabii Kama Musa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
w94 5/1 kur. 3-4

Je! Dini Inatosheleza Mahitaji Yako?

HEWA, maji, chakula, makao—hayo yanatambuliwa ulimwenguni pote kuwa mahitaji ya binadamu. Bila hayo unapungukiwa sana na unaweza kufa. Hata hivyo, zamani za kale kiongozi wa Waisraeli Musa alitaja uhitaji mwingine wa binadamu, uhitaji ulio muhimu hata kuliko chakula au maji. Musa alisema hivi: “Mwanadamu haishi kwa mkate tu, bali huishi kwa kila litokalo katika kinywa cha BWANA.”—Kumbukumbu la Torati 8:3.

Kwa maneno hayo ya maana sana, Musa alionyesha umuhimu wa kutosheleza mahitaji yetu ya kidini au ya kiroho. Yeye alionyesha kwamba uhai wetu wenyewe wategemea kutosheleza mahitaji hayo! Wakati wa safari yao ya miaka 40 jangwani, Waisraeli waliishi kihalisi kwa ‘maneno yatokayo katika kinywa cha Yehova.’ Waliokoka hali ambayo ingewaua. Kwa amri ya Mungu, chakula kiitwacho mana kilianguka kimuujiza kutoka mbinguni. Maji yalitoka kwenye miamba ili yaizime kiu yao. Lakini Mungu aliwafanyia mambo mengi zaidi ya kutunza mahitaji yao ya kimwili. Musa alisema hivi: “Kama vile baba amrudivyo mwanawe, ndivyo BWANA, Mungu wako, akurudivyo.”—Kumbukumbu la Torati 8:4, 5; Kutoka 16:31, 32; 17:5, 6.

Waisraeli hawakuachwa wajitegemee kwa habari ya kujua mema na mabaya, kiadili au kidini. Waliongozwa na Mungu mwenyewe. Aliwapa Sheria ya Kimusa, kanuni ya sheria yenye kutokeza sana iliyotia ndani lishe bora, kanuni kali za usafi, na kanuni bora za kiadili na za kidini. Kwa hiyo Mungu aliendeleza hali-njema ya kiafya na ya kiroho ya Israeli. Waliishi kwa ‘maneno yatokayo katika kinywa cha Yehova.’

Hivyo, Israeli likawa tofauti sana na mataifa mengine. Katika siku za Musa, Misri ilitawala ikiwa mamlaka ya ulimwengu yenye nguvu zaidi. Ilikuwa nchi ya kidini sana. World Book Encyclopedia yasema hivi: “Wamisri wa kale waliamini kwamba viabudiwa vingi (vya kiume na vya kike) vilikuwa na uvutano juu ya kila sehemu ya maumbile na utendaji wa binadamu. Kwa hiyo waliabudu miungu mingi. . . . Katika kila jiji na mji wa Misri, watu waliabudu miungu yao ya kipekee kwa kuongezea miungu wakuu zaidi.”

Je! ibada hiyo ya miungu mingi ilitosheleza mahitaji ya kiroho ya Wamisri? La. Misri ikawa nchi yenye ushirikina sana na yenye mazoea ya ngono zilizopotoka. Badala ya kuendeleza maisha na afya nzuri, njia ya maisha ya Wamisri ilitokeza ‘maradhi mabaya.’ (Kumbukumbu la Torati 7:15) Basi, si ajabu kwamba Biblia ilitaja miungu ya Misri kwa madharau, ikiiita “sanamu-mavi.”—Ezekieli 20:7, 8, New World Translation.

Kuna hali inayofanana na hiyo leo. Watu wengi wana angalau imani fulani ya kidini; watu wachache waweza kujiita kuwa wasioabudu mungu yeyote. Lakini ni wazi kwamba dini kwa ujumla imeshindwa kutosheleza mahitaji ya kiroho ya wanadamu. Je! matatizo ya vita, ubaguzi wa rangi, njaa kali, na ufukara usiokoma yangekuwako leo kama watu wangekuwa kwa kweli wanaishi ‘kwa kila neno litokalo kwa kinywa cha Yehova’? Bila shaka sivyo! Hata hivyo, ni watu wachache wangefikiria kubadili dini yao. Kwani, watu fulani hata hawataki kujadili juu ya dini au kufikiria mawazo mapya ya kidini!

Kwa kielelezo, mtu mmoja nchini Ghana, Afrika Magharibi, aliambia mhudumu Mkristo hivi: “Naamini kwamba Mungu amejifunua kwetu sisi Waafrika kupitia makuhani na makuhani wetu wa kike wenye nguvu sana, kama vile alivyojifunua kwa Wayahudi kupitia manabii wao. Inasikitisha kwamba baadhi yetu sisi Waafrika tunashindwa kutambua makuhani wetu wenyewe na badala ya hivyo twazungumza juu ya Yesu, Muhammad, na watu wengine.”

Katika jumuiya nyingi za kidesturi za Kiafrika, Ukristo huonwa kuwa dini ya wazungu—kitu kilicholetwa ambacho kimetokeza madhara mengi kuliko mazuri. Lakini, je, kukataa kufikiria mawazo mengine kutakusaidia au kutazuia jitihada zako za kutosheleza mahitaji yako ya kiroho? Methali moja ya Kiafrika yasema hivi: “Huwezi kutumbukiza mikono yote miwili ndani ya bakuli la chakula kwa sababu tu una njaa.” Si ungwana kula kwa njia hiyo na vilevile kwaweza kuhatarisha—hasa kama hujui kilichomo ndani ya bakuli! Lakini, watu wengi huchagua dini zao kwa msingi wa hisia au desturi ya familia yao, bali si kwa uchunguzi wa makini.

Ibada inayotosheleza mahitaji yako ya kiroho yapaswa iwe “utumishi mtakatifu pamoja na nguvu zenu za kufikiri.” (Warumi 12:1, NW) Inapaswa iwe ibada iliyochaguliwa baada ya kupata habari na inayopatana na akili. Kwa hiyo, ebu tuchunguze suala la kuchagua dini kutokana na maoni ya Kiafrika. Lakini, mambo yafuatayo yatapendeza wasomaji wa kila mahali.

[Picha katika ukurasa wa 3]

Musa alionyesha umuhimu wa kutosheleza uhitaji wetu wa kiroho

[Picha katika ukurasa wa 4]

Mambo yaliyopata Afrika kutokana na wamishonari wa Jumuiya ya Wakristo yamefanya wengine wakatae kusikiliza Biblia

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki