Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w94 8/15 uku. 32
  • Michoro Yenye Maana ya Pekee

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Michoro Yenye Maana ya Pekee
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
w94 8/15 uku. 32

Michoro Yenye Maana ya Pekee

“IEHOVA SIT TIBI CUSTOS”

MANENO haya yaliyochorwa kwenye ukuta wa mbele wa nyumba ya karne ya 17 katika Celerina, mashariki mwa Uswisi, yamaanisha “Yehova awe mlinzi wako.” Katika sehemu hii ya milima-milima, ni jambo la kawaida kupata jina la Mungu likiwa limechorwa au kuandikwa kwa rangi kwenye nyumba, makanisa, na majumba ya makasisi yenye umri wa karne kadhaa. Jina Yehova lilikuja kujulikanaje sana hivyo?

Rhaetia ya kale (iliyotia ndani sehemu ambazo sasa ni kusini-mashariki mwa Ujerumani, Austria, na Mashariki mwa Uswisi) ilikuja kuwa mkoa wa Roma katika 15 K.W.K. Wakaaji walikuja kusema Kiromanshi (mchanganyiko wa Kirhaetia na Kiroma), lugha yenye msingi wa Kilatini iliyositawi ikawa na lahaja kadhaa ambazo zingali zinasemwa katika baadhi ya mabonde ya milima Alp ya Uswisi na kaskazini mwa Italia.

Baadaye, sehemu za Biblia zilitafsiriwa katika Kiromanshi. Chapa moja, Biblia Pitschna, ilikuwa na Zaburi na Maandikio ya Kigiriki ya Kikristo. Katika Biblia hii, iliyotangazwa katika 1666, jina Iehova ilionekana mara nyingi kotekote katika Zaburi. Kwa kuwa Biblia ilikuwa ndicho kitabu cha msingi cha kusomwa nyumbani, wasomaji wa Biblia Pitschna walikuja kufahamiana na jina la Muumba.

Hata hivyo, vizazi vilivyofuata viliacha kupendezwa na mambo yanayohusu Biblia. Wengi hawakujali kuuliza maana ya neno “Iehova,” wala makasisi hawakujaribu kueleza maana yalo. Kwa hiyo michoro hiyo ikaja kuwa mapambo tu yaliyokuwa kawaida ya enzi iliyopita.

Katika miongo ya karibuni badiliko lenye kutokeza katika uelewevu limetukia. Mashahidi wa Yehova wamesafiri kutoka nyanda za chini, wakitumia malikizo katika mabonde haya yenye kupendeza na kujitahidi kuwafundisha wakaaji juu ya yule Mungu ambaye jina lake ni Yehova. Mashahidi wengine wamefanya makao katika eneo hilo ili waweze kutumia wakati mwingi zaidi wakiongea na watu juu ya makusudi mazuri ajabu ya Muumba kuelekea dunia na mwanadamu. Hivyo, michoro hiyo ya kale ya Kiromanshi yanapata umaana mpya watu wapatapo kujifunza juu ya Mungu wa kweli, Yehova.

[Picha katika ukurasa wa 32]

IEHOVA PORTIO MEA: Yehova ndiye fungu langu. —Ona Zaburi 119:57

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki