“Nimeumbwa kwa Jinsi ya Ajabu”
“NILITOKA wapi?” Hili ni swali ambalo wengi wa watoto wachanga huuliza wakati mmoja au mwingine. Watoto wakuapo, mara nyingi swali lao huja kuwa la kindani sana: “Uhai ulitoka wapi?” Swali hilo limejadiliwa kwa maelfu ya miaka, na kwa wakati huu wanasayansi wengi huona mageuzi kuwa jibu lifaalo zaidi kwa fumbo hilo la chanzo cha uhai. Kwa msingi, maelezo ya mwanamageuzi ni kwamba uhai ulianza wenyewe tu.
Karibu miaka 3,000 iliyopita, Mfalme Daudi aliandika hivi: “Nimeumbwa kwa jinsi ya ajabu ya kutisha.” (Zaburi 139:14) Kadiri tujifunzavyo juu ya uhai, ndivyo tunavyoona ukweli wa maneno hayo. Kwa kweli, mwanafizikia Fred Hoyle aliandika hivi: “Wanakemia na biolojia wagunduapo mambo mengi zaidi juu ya utata wa maisha, inakuwa wazi kwamba uwezekano wao wa kuanza wenyewe kwa aksidenti fulani ni mdogo sana hivi kwamba huo waweza tu kupuuzwa. Uhai haungeanza peke yao tu.”
Kwa hiyo, ni nini chanzo cha uhai? Makala mbili za kwanza za gazeti hili zajadili swali hilo. Ikiwa ungependa habari zaidi, tafadhali andikia I.B.S.A., Box 47788, Nairobi, Kenya, au tumia anwani ifaayo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa 2.