Unaalikwa kwa Moyo Mweupe
Kifo cha mwanamume Yesu Kristo zaidi ya miaka 1,900 iliyopita kilikuwa tukio la maana zaidi katika historia. Kilifungulia matazamio ya kupata uhai wa milele katika hali za paradiso. Wakati wa sherehe sahili moja, Yesu alitumia divai na mkate usiotiwa chachu kuwa mifano ya dhabihu yake ya kibinadamu yenye upendo. Halafu akawaambia wanafunzi wake: “endeleeni kufanya hivi katika kunikumbuka mimi.” (Luka 22:19, NW) Je, wewe utakumbuka tukio hili muhimu? Mashahidi wa Yehova wanakualika kwa uchangamfu ujiunge nao katika kufanya mwadhimisho huo wa ukumbusho. Utakuwa baada ya jua kushuka katika tarehe inayolingana na nisani 14 kwenye kalenda-mwezi ya Biblia. Unaweza kuhudhuria kwenye Jumba la Ufalme lililo karibu zaidi nawe. Tafuta kujua kutoka kwa Mashahidi wa Yehova wa kwenu kuhusu wakati na mahali barabara. Tarehe ya mwadhimisho katika 1995 itakuwa Ijumaa, Aprili 14.